Naibu Waziri wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA,
akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya
Utangazaji unaoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA,
akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya
Utangazaji unaoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika
Ukumbi wa New Generation jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA, akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji unaoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika Ukumbi wa New Generation jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA, akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji unaoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Na Mwandishi Wetu
Serikali
imepunguza kwa kiasi kikubwa ada za maombi ya leseni kwa vyombo vya
habari mtandaoni, kutoka shilingi laki tano hadi 50,000= huku ada ya
maombi ikiwa shilingi 10,000/= tu kutoka shilingi 50,000/= hatua
inayotajwa kuwa mkombozi kwa wanahabari na wamiliki wa blogu na Online
Tv nchini.
Hatua
hiyo imetangazwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA, wakati akifungua
rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji unaoandaliwa na
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika Ukumbi wa New Generation
jijini Dodoma.
Mbali
na kupunguza ada hizo, Mwinjuma ameielekeza TCRA kushirikiana na Bodi
ya Ithibati kuhakikisha wafanyakazi wa vyombo vya habari wanalipwa
stahiki zao kwa wakati, wakiwemo wale wanaodai mishahara ya zaidi ya
miezi sita.
Amesisitiza kuwa ndani ya wiki moja anatarajia kupokea mrejesho wa hatua zilizochukuliwa kuhusu suala hilo.
Amesema
Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea
kuboresha mazingira ya ufanyaji kazi kwa vyombo vya habari, huku
akisisitiza umuhimu wa ubora wa maudhui, kuzingatia maadili ya taaluma
na kulinda haki miliki.
“Haki
ya kupata taarifa ni ya kila Mtanzania, hivyo vyombo vya habari
vinapaswa kuwafikia wananchi wote bila upendeleo,” amesisitiza.
Aidha,
amesema Wizara itaendelea kuimarisha mazingira ya sekta hiyo ili
wananchi wa vijijini wanufaike na huduma za utangazaji kwa urahisi,
sambamba na kuhimiza matumizi ya teknolojia za kisasa ikiwemo Akili Unde
(AI) kwa tija.
Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Watangazaji Huru Tanzania (NIBA),
Amos Ngosha, ameomba Serikali kupunguza wingi wa tozo zinazoikabili
sekta hiyo, akieleza kuwa vyombo vya habari hulipa zaidi ya tozo 19 kila
mwaka chini ya sheria tofauti, hali inayodhoofisha uwezo wao kifedha na
kusababisha baadhi kushindwa kuendelea na huduma au kufungiwa.
Naye
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabir Bakari, amesema mwaka 2025 jumla ya
wanahabari 2,054 wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo, huku usikivu
wa redio ukifikia asilimia 85 na usambazaji wa televisheni kupitia
satelaiti kufikia asilimia 100.
Hadi
Desemba 2025, jumla ya leseni 770 za utangazaji zilikuwa zimetolewa,
huku TCRA ikiwa na mpango wa kuanzisha mfumo wa redio kidijitali ili
kuendana na maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya soko la mawasiliano.
Mkutano
huo wa siku mbili, unaofanyika Februari 12 na 13, 2026, umewakutanisha
viongozi na wadau wa sekta ya utangazaji kujadili namna ya kuimarisha na
kupanua huduma za utangazaji nchini.









No comments:
Post a Comment