Wednesday, August 20, 2025

NAPLES ZOO YATOA MSAADA WA MAHEMA KUSAIDIA UHIFADHI WA FARU WEUPE NGORONGORO






Katika kuendeleza juhudi za kuimarisha uhifadhi na ulinzi wa rasilimali za wanyamapori, Taasisi ya Caribbean Naples Zoo kutoka Marekani imetoa msaada wa mahema kumi (10) kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Msaada huu una lengo la kuimarisha shughuli za uhifadhi wa faru weupe na wanyama wengine waliopo katika eneo la urithi wa dunia la Ngorongoro.

Mwakilishi wa Caribbean Naples Zoo Tanzania, Albert Mollel, ameashiria kuwa msaada wa vifaa hivi ni muendelezo wa ushirikiano wa kimataifa unaolenga kuimarisha ulinzi na uhifadhi endelevu wa wanyamapori, hususan aina adimu na zile zilizo hatarini kutoweka kama faru.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA, Bw. Abdul-Razaq Badru, amemshukuru Caribbean Naples Zoo kwa msaada huu muhimu. Pia alisisitiza kuwa vifaa hivyo vitawawezesha askari wa uhifadhi kufanya kazi kwa ufanisi zaidi katika kulinda faru na wanyama wengine waliopo Hifadhi ya Ngorongoro

No comments:

RAIS SAMIA AENDELEZA DIPLOMASIA YA KIMATAIFA DUBAI, ALAKIWA NA MAZUNGUMZO NA MTAWALA WA DUBAI KANDO YA WGS 2026

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan , ameendelea kuimarisha diplomasia ya kimataifa kwa kufanya m...