Wednesday, August 20, 2025

NAPLES ZOO YATOA MSAADA WA MAHEMA KUSAIDIA UHIFADHI WA FARU WEUPE NGORONGORO






Katika kuendeleza juhudi za kuimarisha uhifadhi na ulinzi wa rasilimali za wanyamapori, Taasisi ya Caribbean Naples Zoo kutoka Marekani imetoa msaada wa mahema kumi (10) kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Msaada huu una lengo la kuimarisha shughuli za uhifadhi wa faru weupe na wanyama wengine waliopo katika eneo la urithi wa dunia la Ngorongoro.

Mwakilishi wa Caribbean Naples Zoo Tanzania, Albert Mollel, ameashiria kuwa msaada wa vifaa hivi ni muendelezo wa ushirikiano wa kimataifa unaolenga kuimarisha ulinzi na uhifadhi endelevu wa wanyamapori, hususan aina adimu na zile zilizo hatarini kutoweka kama faru.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA, Bw. Abdul-Razaq Badru, amemshukuru Caribbean Naples Zoo kwa msaada huu muhimu. Pia alisisitiza kuwa vifaa hivyo vitawawezesha askari wa uhifadhi kufanya kazi kwa ufanisi zaidi katika kulinda faru na wanyama wengine waliopo Hifadhi ya Ngorongoro

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...