KAMISHNA BADRU ATAKA UBUNIFU ILI KUENDELEZA MAPANGO YA AMBONI
Na Hamis Dambaya, Amboni Tanga.
Kamishna wa Uhifadhi Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Abdul-razaq Badru amesema mamlaka hiyo Kwasasa itajikita katika kuendeleza ubunifu ili mapango ya Amboni yaliyoko mkoani Tanga yaweze kuvutia wageni wengi kutoka ndani na nje ya Nchi
Katika mazungumzo yake na watendaji wa kituo hicho Kamishna Badru amesema eneo hilo ni hazina na kinachohitajika ni kulitumia kama fursa ya kiuchumi kupitia shughuli za utalii.
“Tushirikiane kwa umoja wetu na tubuni miradi ambayo italifanya eneo la Amboni liwe na mvuto kwa wageni wetu kutoka ndani na nje ya nchi,”alisema Kamishna Badru.
Mapango ya Amboni yamebeba hazina yenye historia mbalimbali ikiwemo harakati za kudai uhuru wa Tanzania bara,urithi na utamaduni wa makabila na watu wa Tanga pamoja na mafunzo ya jiografia ambapo ni adimu kupatikana katika nchi nyingine duniani.
No comments:
Post a Comment