Thursday, August 21, 2025

Rais Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha CCM chaguo la wagombea bunge






Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kilichofanyika leo, Agosti 21, 2025, Jijini Dodoma.

Kikao hiki kililenga kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za kisiasa, ikiwa ni pamoja na:

  • Wagombea Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

  • Wabunge wa Viti Maalum,

  • Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, na

  • Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Viti Maalum.

Rais Samia Suluhu Hassan aliwashirikisha wajumbe wa kikao hiki mchakato wa kikatiba na uwajibikaji wa kuchagua wagombea wenye sifa bora, ili kuhakikisha uwakilishi unaoendana na matarajio ya wananchi na maendeleo ya taifa.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...