Saturday, April 01, 2017

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC)

1
Kufuatia uteuzi wa Bibi Blandina S.J. Nyoni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) tarehe 25/02/2017.  Mhe. William V. Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 5(2) cha Sheria Na. 2 ya Mwaka 1990, amewateua Wajumbe 7 wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa.
Aidha, uteuzi huu ni wa kipindi cha miaka mitatu (3), kuanzia tarehe 23 Machi, 2017.
 Majina ya wajumbe hao ni kama ifuatavyo:
  1. Prof. John M. Lupala
  2. Bwn. Gabriel Malata
  3. Bi. Mary Mlay
  4. Bi. Subira Mchumo
  5. Bwn. Ally Hussein Laay
  6. Bwn. Pius Maneno
  7. Bwn. Kesogukwele Masudi Issa Miraji Msita
Imetolewa na:
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

No comments:

SAMIA APEPERUSHA BENDERA YA USHIRIKIANO EAC, AKUTANA NA KATIBU MKUU IKULU CHAMWINO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ...