
Kufuatia uteuzi wa Bibi Blandina S.J. Nyoni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) tarehe 25/02/2017.  Mhe. William V. Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 5(2) cha Sheria Na. 2 ya Mwaka 1990, amewateua Wajumbe 7 wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa.
Aidha, uteuzi huu ni wa kipindi cha miaka mitatu (3), kuanzia tarehe 23 Machi, 2017.
 Majina ya wajumbe hao ni kama ifuatavyo:
- Prof. John M. Lupala
 - Bwn. Gabriel Malata
 - Bi. Mary Mlay
 - Bi. Subira Mchumo
 - Bwn. Ally Hussein Laay
 - Bwn. Pius Maneno
 - Bwn. Kesogukwele Masudi Issa Miraji Msita
 
Imetolewa na:
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
No comments:
Post a Comment