Saturday, April 22, 2017

Mkutano wa CUF Wavamiwa na Watu Wasiojulikana


Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad.
Watu wasiojulikana wakiwa na bastola wamevamia mkutano wa wanachama wa CUF ambao unamuunga mkono, Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na kushusha kipigo kwa baadhi ya wananchama wa CUF na waandishi wa habari.

Mtu mmoja miongoni mwa waliovamia mkutano wa wanachama wa CUF ameshambuliwa na wananchi wakati akijaribu kutoroka.

Mkutano huo ambao ulikuwa na lengo la kumtambulisha Katibu Mkuu wa CUF, inadaiwa watu hao waliovamia mkutano huo na kufanya vurugu ni wanachama wa Cuf ambao wanamuunga mkono Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.
Kwa mujibu wa taarifa zilizokuwepo mkutano huo ulipangwa kufanyika majira ya saa tano za asubuhi katika hoteli ya Vina, Mabibo lakini kabla ya kuanza waliibuka watu hao wasiojulikana wakiwa wamevalia soksi nyeusi usoni kuficha sura zao na kususha kipigo kwa baadhi ya wanachama wa CUF waliokuwepo katika eneo hilo na waandishi wa habari.

No comments:

NHC YATOA ELIMU YA HATI PACHA, YASISITIZA UMOJA WA WAMILIKI SAMIA HOUSING SCHEME KAWE

 Samia Housing Scheme Kawe: nyumba 560, familia tofauti zikiunganishwa na mtindo mmoja wa maisha ya  kisasa—ushirikiano, ustaarabu na “moder...