Thursday, April 27, 2017

RAIS MAGUFULI KUWA MGENI RASMI SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

Mwakilishi wa Jukwaa la Wahariri Nchini, Neville Meena ambaye alikuwa mshereheshaji wa Mkutano huo akizungumza Jambo.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa Siku ya Uhuru wa Vyombo Vya Habari itakapofanyika Mei 2,3 mwaka huu.
Afisa Maudhui kutoka Tanzania Media Fund (TMF ), Raziah Mwawanga naye akizungumza Jambo.
Mdau akifafanua jambo.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Salome Kitomari amesema kuwa maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Malaika Beach Resort iliyoko jijini Mwanza.
Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
Akielezea juu ya maadhimisho hayo amesema kuwa wanatarajiwa kuwepo wadau mbalimbali na kutaweza kuzungumzwa masuala yanayohusu Uhuru wa vyombo vya Habari na wanahabari kwa ujumla.

No comments: