Sunday, September 21, 2025

Makamu wa Rais Dkt. Mpango Awasili Marekani kwa Kikao cha UNGA 80











Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, leo tarehe 21 Septemba 2025 amewasili jijini New York, Marekani.

Dkt. Mpango yupo nchini humo kwa ajili ya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA 80).

Tanzania kupitia ushiriki huu inaendelea kushirikiana na mataifa mbalimbali duniani katika kujadili masuala muhimu ya maendeleo, diplomasia, uchumi na ustawi wa dunia.


Tanzania mbele kwenye majukwaa ya kimataifa!



No comments:

TARURA YATEKELEZA UJENZI WA KM 56 ZA BARABARA ZA LAMI ILALA KUPITIA DMDP II

‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza kutekeleza ujenzi wa barabara zaidi ya Kilomita 56 kwa kiwango...