Sunday, September 21, 2025

Makamu wa Rais Dkt. Mpango Awasili Marekani kwa Kikao cha UNGA 80











Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, leo tarehe 21 Septemba 2025 amewasili jijini New York, Marekani.

Dkt. Mpango yupo nchini humo kwa ajili ya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA 80).

Tanzania kupitia ushiriki huu inaendelea kushirikiana na mataifa mbalimbali duniani katika kujadili masuala muhimu ya maendeleo, diplomasia, uchumi na ustawi wa dunia.


Tanzania mbele kwenye majukwaa ya kimataifa!



No comments:

WAZIRI MKUU: FEDHA ZA MUUNGANO ZITUMIKE KUKARABATI MIUNDOMBINU YA BARABARA

  WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza fedha ...