Monday, September 29, 2025

REA yauza majiko 1,500 kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho ya Madini Geita



๐Ÿ“ŒREA yapongezwa kwa kuuza majiko kwa bei ya ruzuku na kutoa elimu ya miradi ya wakala

๐Ÿ“Geita

Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita yamehitimishwa rasmi na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambayo yalifunguliwa Septemba 18 na kufikia kilele tarehe 28 Septemba, 2025

Wakala umeshiriki maonesho hayo kwa kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia, kutoa elimu ya miradi inayotekelezwa na wakala wa nishati vijijini pamoja na fursa zinazopatikana kwa wakala kama vile vituo vidogo vya mafuta.

Sambamba na hayo Wakala unahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuuza kwa ruzuku mitungi ya gesi ya kilo 6 ambayo inauzwa kwa bei ya 50% ambayo ni kiasi cha shilingi 17,500 ambapo jumla ya mitungi 5,00 imeuzwa kwa ruzuku kwenye maonesho.

Pamoja na hayo, Wakala unafadhili uuzwaji wa majiko banifu yanayotumia mkaa mbadala pamoja na mkaa wa kawaida, majiko hayo yameuzwa kwa bei ya ruzuku ya 85% ambayo ni shilingi 6,195 ambapo bei yake ya kawaida ni shilingi 41,300 ambapo majiko banifu 1,000 yatauzwa kwa bei ya ruzuku katika maonesho hayo. 

Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini 2025  yamefanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili mkoani Geita.

No comments:

TARURA YATEKELEZA UJENZI WA KM 56 ZA BARABARA ZA LAMI ILALA KUPITIA DMDP II

‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza kutekeleza ujenzi wa barabara zaidi ya Kilomita 56 kwa kiwango...