Tuesday, September 30, 2025

TANAPA YAMPONGEZA SIMBU; YAAHIDI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NAE KUTANGAZA HIFADHI ZA TAIFA KUPITIA MCHEZO WA RIADHA










Na. Philipo Hassan, Arusha

Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, CPA Musa Nassoro Kuji, amempongeza rasmi Sajini Taji Alphonce Simbu, bingwa wa Dunia katika mbio ndefu za kilometa 42 mwaka 2025, akisisitiza kuendelea kushirikiana naye katika jitihada za kutangaza hifadhi za taifa kupitia michezo ya riadha. Pongezi hizo zimetolewa Makao Makuu ya TANAPA, jijini Arusha, katika hafla iliyohudhuriwa na Menejimenti ya Shirika pamoja na waandishi wa habari.

Sajini Taji Simbu aliibuka mshindi wa medali ya dhahabu katika mashindano ya mbio ndefu yaliyofanyika nchini Japan kuanzia Septemba 13 hadi Septemba 21, 2025, matokeo ambayo yameipa Tanzania heshima kubwa katika jukwaa la kimataifa.

“Tunakupongeza sana Simbu kwa jitihada na bidii ulizozionyesha katika kuipambania Bendera ya Taifa letu. Ushindi huu si tu ni ushindi wa kibinafsi, bali ni utambulisho mkubwa wa taifa letu duniani,” alisema Kamishna Kuji, akiashiria umuhimu wa michezo katika kuimarisha taswira ya Tanzania kimataifa.

Aidha, Kamishna Kuji alisisitiza kuwa TANAPA iko tayari kushirikiana na wanamichezo wa kitaifa na kimataifa, si tu katika kutangaza hifadhi za taifa bali pia katika kukuza utamaduni wa michezo na maisha yenye afya. “Kupitia michezo kama mbio ndefu, wanamichezo wanakuwa mabalozi wa hifadhi zetu, wakionyesha uzuri wa maliasili na vivutio vya utalii vya Tanzania,” alisema.

Hafla hiyo pia ilijumuisha wawakilishi wa sekta ya michezo, wadau wa utalii, na waandishi wa habari, ikionyesha uwepo wa mshikamano wa jamii katika kuenzi mafanikio ya wanamichezo na umuhimu wa michezo kama njia ya matangazo ya hifadhi na taifa.

Sajini Taji Simbu, kwa upande wake, aliishukuru TANAPA kwa pongezi hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana na wadau wa hifadhi na michezo, akisisitiza kuwa mafanikio yake ni matokeo ya jitihada za pamoja, moyo wa taifa, na msaada kutoka kwa wadau wa michezo na hifadhi nchini.

VIWANGO VYA UDUMAVU NA UKONDEVU VIMEPUNGUA NCHINI-MAJALIWA







Asema Serikali kuwa lishe ni nguzo ya maendeleo ya rasilimali watu, uchumi na jamii

Asema kiwango cha uzito uliozidi na uzito kupita kiasi hasa wanawake wa umri wa kuzaa kimeongezeka

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa kiwango cha udumavu miongoni mwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano nchini kimeshuka kutoka asilimia 48 mwaka 1992 hadi asilimia 30 mwaka 2022. 

Ameongeza kuwa, kiwango cha ukondefu miongoni mwa watoto walio chini ya miaka mitano kimepungua kutoka asilimia 5 mwaka 1992 hadi asilimia 3.2 mwaka 2022.

Amesema hayo leo Jumanne (Septemba 30, 2025) wakati alipofunga mkutano wa 11 wa wadau wa lishe nchini, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa APC uliopo Bunju Jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua kuwa lishe si suala la kiafya pekee, bali ni nguzo ya maendeleo ya rasilimali watu, uchumi na jamii. “Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na chakula cha kutosha, afya njema na lishe bora”

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameendelea kuwa kinara wa mapambano dhidi ya utapiamlo kwa kuhakikisha masuala ya lishe yanapewa kipaumbele kwa kuimarisha bajeti, kuboresha mifumo ya ufuatiliaji na uhamasishaji wa afua za lishe kuanzia ngazi ya taifa hadi vijijini.

 “Jitihada hizi zilimuwezesha kupata tuzo ya Global Goalkeeper kutoka Taasisi ya Gates Foundation, kutokana na mchango wake mkubwa katika kusukuma mbele Malengo ya Maendeleo Endelevu, hususan kwenye afya ya mama, mtoto na lishe”.

Katika hatua nyingine, mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa kiwango cha uzito uliozidi na uzito kupita kiasi (kiribatumbo) hasa miongoni mwa wanawake wa umri wa kuzaa kimeongezeka kutoka asilimia 28 mwaka 2015 hadi asilimia 37 mwaka 2022. “Changamoto hii inaakisi mabadiliko ya ulaji na mtindo wa maisha ulioikumba sio tu Tanzania bali dunia nzima“.

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Wizara na Taasisi zote za umma na binafsi kutenge rasilimali za kutosha kwa ajili ya afua za lishe na kuziweka katika mipango yao ya kila mwaka ili kuongeza uwajibikaji na uendelevu katika kutekeleza mipango iliyopangwa.

Pia Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Utafiti na Vyuo vya Elimu ya juu kuendeleza tafiti katika masuala ya lishe pamoja na kuhakikisha ripoti za tafiti hizo zinatumika kuboresha sera na mikakati nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu)Ridhiwan Kikwete amesema kuwa Serikali itahakikisha kuwa wadau wote walioanishwa katika Mpango Jumuishi wa masuala ya Lishe wanaendela kutekeleza majukumu yao. "Hii ni pamoja na kuhakikisha kuwa Wizara zote zinaingiza masuala ya lishe katika mipango ya kibajeti kila mwaka"

Ameongeza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imefanikiwa kukamilisha zoezi la utafiti wa gharama za utapiamlo ambao ulilenga kubainisha gharama na athari za utapiamlo katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi

"Matokeo ya utafiti huo yatatumika kama nyenzo muhimu ya uhamasishaji wa viongozi wa juu wa Serikali na watunga sera, kupitia majukwaa mbalimbali ili kuchangia hatua zaidi katika mapambano ya kutokomeza utapiamlo hasa kwa watoto"

NGORONGORO YAENDELEA NA KUBORESHA HUDUMA YA MAJI SAFI NA MIUNDOMBINU KWA AJILI YA WANANCHI.



Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii  imetembelea kijiji cha Olpiro kilichopo Kata ya Eyasi, wilayani Ngorongoro, na kuchukua hatua za kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi pamoja na mifugo yao.

Wataalam kutoka NCAA katika ziara iliyofanyika  Septemba 30, 2025, wamekagua marekebisho na ukarabati wa miundombinu ya maji uliofanyika katika kijiji hicho, hatua iliyowawezesha wananchi kupata huduma ya maji safi na salama.

Ukarabati wa miundombinu  ya huduma ya maji katika kijiji hicho umeleta faraja kubwa kwa wananchi hao waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji kwa muda mrefu.

Aidha, pamoja na maboresho ya huduma ya maji, NCAA pia imefanya tathmini ya miundombinu mingine ikiwemo josho la kuogeshea mifugo lililopo katika kijiji hicho.

Wananchi wa kijiji cha Olpiro wameipongeza Serikali kupitia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kwa jitihada hizo wakieleza kuwa zinachangia sio tu katika kuboresha maisha yao ya kila siku, bali kulinda afya zao na kuendelea kuunga mkono Serikali katika  shughuli za uhifadhi.

KATI YA MLIMA NA MJI, 2H YASIMAMA KAMA NEMBO MPYA YA MOROGORO

 





2H si jengo tu, bali ni alama ya maendeleo na uthubutu

Na Mwandishi Wetu

Katika moyo wa Jiji la Morogoro, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeandika ukurasa mpya wa maendeleo kupitia kukamilika kwa hatua muhimu ya mradi wa jengo la kisasa la biashara na makazi lililojengwa katika Kiwanja Na. 2, Block H, Lumumba Street, katikati ya Manispaa ya Morogoro.

Mradi huu, unaojulikana kama 2H – Morogoro Project, si tu sehemu ya ujenzi wa jengo jipya, bali ni mfano wa dira pana ya maendeleo ya miji nchini Tanzania, ambapo makazi bora, biashara za kisasa na ustawi wa kijamii vinaunganishwa kwa ustadi mkubwa.

Jengo hili limebuniwa na kuidhinishwa na timu ya wabunifu wa NHC, likiwa na mpangilio wa kisasa unaolenga kutosheleza mahitaji ya makazi ya familia, wajasiriamali na wafanyabiashara.

Ndani ya jengo hili, kumepangwa aina mbalimbali za makazi ili kuhakikisha kila kundi la watu lina nafasi ya kuishi au kufanya kazi kwa mazingira bora. Studio apartments zenye ukubwa wa takribani mita za mraba 39 zimeundwa kwa ajili ya wanafunzi, wataalamu wachanga na watu binafsi wanaohitaji makazi yenye urahisi na gharama nafuu lakini yenye ubora na usasa.

Aidha, nyumba ya chumba kimoja cha kulala kinachotofautiana kati ya mita za mraba 47 hadi 66 vimeundwa kwa ajili ya familia ndogo au watu wanaopendelea faraja zaidi pamoja na nafasi za mapumziko, huku nyumba ya vyumba viwili vya kulala vyenye ukubwa wa mita za mraba 100 zikitoa makazi yenye nafasi kubwa, mwonekano wa kisasa na mpangilio bora wa ndani kwa familia kubwa zaidi.

Zaidi ya hapo, kila ghorofa limewekewa eneo la pamoja lenye zaidi ya mita za mraba 86, ambapo wakazi na wageni wanaweza kufurahia hewa safi, kupumzika au kushiriki shughuli za kijamii, jambo linaloongeza mshikamano wa kijamii na kuimarisha ubora wa maisha ndani ya jengo.

Kwa mtu ambaye hajawahi kufika kwenye eneo hili, picha ya jengo la 2H ni ya kuvutia na ya kusisimua. Unapopanda ngazi, unakutana na lobby kubwa yenye mwanga wa kutosha, ikionekana kama mlango wa kisasa wa mapokezi unaoleta heshima kwa kila anayeingia.

Kila ghorofa limebeba muundo uliofikiria kwa makini, ukiunganisha sehemu za chakula iliyounganishwa na sebule, jikoni za kisasa zilizo rahisi kutumia na vyoo vya kisasa vilivyowekwa kwa ustadi mkubwa. Aidha, balcony zilizowekwa kwa mpangilio wa kuvutia zinatoa mandhari ya kipekee ya anga la Morogoro, jambo linaloongeza thamani ya kila chumba na kumfanya mkazi kuhisi kuwa yupo katika makazi ya kiwango cha juu.

Mradi huu ulianza rasmi mwezi Juni 2024 na unatarajiwa umekamilika mwezi Septemba 2025, ukiwa na bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5. Hadi sasa, maendeleo ya ujenzi yamefikia asilimia 97, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4 katika kipindi cha hivi karibuni.

Hii ni dalili kwamba kazi imefanyika kwa kasi na nidhamu kubwa, huku kila sakafu inayoongezwa ikileta matumaini mapya kwa wakazi wa Morogoro. Hatua hii ilishuhudiwa wazi pale ambapo Wakandarasi wa NHC walikabidhi sehemu kubwa ya kazi kwa Meneja wa NHC Mkoa wa Morogoro, Eliaisa Keenja, jambo linaloonyesha kuwa mradi huu uko katika mstari wa ukamilishaji na tayari umeanza kutoa matunda yanayoonekana kwa macho.

Akizungumza kuhusu mradi huu, Mkurugenzi wa Ujenzi wa NHC, Dkt. Godwin Maro, amesema: “Mradi wa 2H Morogoro ni ushahidi wa dhamira ya NHC katika kusimamia ujenzi wa majengo ya viwango vya juu vinavyoendana na mabadiliko ya kisekta na kasi ya ukuaji wa miji yetu. Tumetumia utaalamu wa kisasa kuhakikisha jengo hili si tu linakidhi mahitaji ya sasa, bali pia linaweza kuhimili mahitaji ya baadaye. Ni jengo lililojengwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uimara, usalama na uendelevu, na tunaliona kama kielelezo cha namna Shirika linavyoshiriki kwa dhati katika kubadilisha sura ya makazi na biashara nchini Tanzania.” 

Umuhimu wa mradi huu unakwenda mbali zaidi ya sura ya jengo lenyewe. Kiuchumi, jengo hili linatarajiwa kuwa chachu ya kuongeza fursa mpya za biashara, ofisi na makazi, hivyo kuchochea mtiririko wa uwekezaji na ajira ndani ya Morogoro.

Kijamii, linatoa makazi bora yenye mazingira salama na ya kisasa, hivyo kuboresha kiwango cha maisha ya wakazi. Kimkakati, linainua hadhi ya Morogoro kama kitovu cha kibiashara, na kuimarisha nafasi yake katika ramani ya maendeleo ya kitaifa.

Kimaono, ni ishara ya nia ya NHC kubadilisha sura ya miji ya Tanzania kutoka makazi ya kizamani kuelekea majengo ya kuvutia yenye uwezo wa kuhimili ongezeko la watu na mahitaji ya kisasa.

Kwa wale ambao hawajawahi kufika Morogoro, jengo hili linaweza kuonekana kama alama ya mabadiliko makubwa. Linavyosimama katikati ya mji, likiwa na ubunifu wa kisasa na mvuto wa kipekee, linatoa picha ya taifa linaloelekea kwenye ustaarabu mpya wa miji.

Hii ndiyo maana NHC imeendelea kushindana na wakati, kwani kila jiwe, kila sakafu na kila mchango unaowekwa ni ushahidi wa ahadi ya kutimiza ndoto ya Watanzania ya kuwa na makazi bora na fursa za biashara zinazochochea maendeleo ya kitaifa.

Kwa ujumla, mradi wa 2H – Morogoro si jengo tu, bali ni alama ya maendeleo na uthubutu. Ni almasi mpya inayong’aa katika sura ya mkoa wa Morogoro, ikiashiria mustakabali wa Tanzania unaoelekea kwenye ustaarabu wa makazi na biashara wa kisasa, unaoshikika, unaoonekana na unaowapa matumaini wananchi wote kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

DKT. SAMIA AHIDI KUKAMILISHA DARAJA LA PANGANI NA BARABARA YA KIMKAKATI BAGAMOYO–SAADANI–PANGANI–TANGA







Na John Bukuku, Tanga 

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuonesha dira ya maendeleo kwa Watanzania baada ya kuahidi kukamilisha ujenzi wa daraja la Pangani na barabara ya Bagamoyo–Saadani–Pangani–Tanga – miradi mikubwa itakayofungua ukanda wa Kaskazini kiuchumi na kuimarisha fursa za utalii na biashara.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika wilayani Pangani, Septemba 29, 2025, Dkt. Samia alisema barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 50 tayari imekamilika kwa asilimia 75, na Serikali imedhamiria kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati.

Aidha, alibainisha kuwa mara tu daraja la Pangani litakapoanza kutumika, wananchi hawatalazimika tena kusafiri umbali mrefu kuunganisha mikoa ya Pwani, Tanga na Kilimanjaro.

“Daraja la Pangani ni mkombozi wa wananchi, na barabara hii ndiyo kiunganishi muhimu cha ukanda huu. Tukikamilisha miradi hii, changamoto za usafiri zitabaki kuwa historia. Nataka kuona wananchi wa Pangani na mikoa jirani wakinufaika moja kwa moja kwa kupanuka kwa biashara, utalii na uwekezaji,” alisema Dkt. Samia huku akishangiliwa na umati wa wananchi.

Dkt. Samia alihimiza wananchi waendelee kuiamini CCM na kumpa kura ya ndiyo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, ili chama hicho kiendelee kusukuma mbele ajenda ya maendeleo yenye kuleta matokeo ya kweli kwa Watanzania wote.

Kwa kauli hiyo, Pangani na ukanda mzima wa Kaskazini unaendelea kupata matumaini mapya ya kimaendeleo kupitia miradi mikubwa ya miundombinu, inayolenga kuunganisha mikoa, kuongeza fursa za kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

Monday, September 29, 2025

Mwili wa Hayati Askofu Mkuu Rugambwa wapokelewa Bukoba







Mwili wa Hayati Askofu Mkuu Novatus Rugambwa, aliyefariki hivi karibuni, uliwasili leo katika Kanisa Kuu la Bikira Maria wa Huruma, Jimbo Katoliki Bukoba, na kupokelewa kwa heshima kubwa na waumini pamoja na viongozi wa Kanisa Katoliki.

Waumini kwa mamia walijitokeza kuupokea mwili huo, huku ibada maalum ya kumuombea ikiongozwa na viongozi wa Kanisa, ikihudhuriwa pia na viongozi wa Serikali, wawakilishi wa madhehebu mbalimbali pamoja na wananchi.

Katika hotuba zao, viongozi wa dini walimsifu Hayati Askofu Mkuu Rugambwa kwa uongozi wake thabiti, hekima, na moyo wa utumishi uliogusa maisha ya wengi, si tu ndani ya Kanisa, bali pia katika jamii kwa ujumla.

Waumini waliendelea kumwombea marehemu apumzike katika amani ya Bwana, huku taratibu za mazishi zikitarajiwa kuendelea katika siku chache zijazo.

DKT. BITEKO AWAPA HEKO WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI



Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Serikali imeongeza ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini ikiwa ni pamoja na shughuli zote za mnyororo mzima wa thamani wa madini nchini ambapo kwa Mkoa wa Geita pekee wachimbaji wadogo wamezalisha kilo 22,014.61 zenye thamani ya shilingi trilioni 3.443 na Serikali kukusanya mapato ya shilingi bilioni 2.5 katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2024/2025.

Mchango wa wachimbaji wadogo wa madini umeongezeka kutoka asilimia 20 mwaka 2020 hadi kufikia asilimia 40 mwaka 2024 katika mapato yote ya sekta ya madini na mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 6.8 mwaka 2020 hadi kufikia asilimia 10 mwaka 2024.

Akizungumza Septemba 28, 2025 katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan Bombambili mkoani Geita wakati akifunga Maonesho ya Nane ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini, yenye kauli mbiu “Ukuaji wa Sekta ya Madini ni Matokeo ya Matumizi ya Teknolojia Sahihi na Uongozi Bora/Shiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025”. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza wachimbaji wadogo na Wizara ya Madini kwa hatua hiyo.

“ Napenda kutoa pongezi maalum kwa Wizara ya Madini kwa usimamizi mzuri wa sekta hii pamoja na wachimbaji wadogo wa Tanzania. Ninyi ni sababu ya kusheherekea mafanikio haya mmekuwa shamba darasa na baada ya Serikali kuwapatia nafasi mmeonesha kwa vitu mlivyofanya mkipewa fursa mnaweza,” Amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea “Mmepambana sana kuleta teknolojia ndani ya nchi na mmeonesha Watanzania wanaweza kufanya mambo makubwa na wakafanikiwa,”

Aidha, amesema kuwa tangu kuanza kwa maonesho hayo mwaka 2018 kumekuwepo na mabadiliko makubwa ya kiteknolojia yanayochangia kuongezeka kwa kasi ya uzalishaji madini hasa kwa wachimbaji madini wadogo. Ambapo katika uchenjuaji madini, zimekuwepo teknolojia mbalimbali za kisasa zikiwemo Carbon – In – Leach (CIL), Carbon – In – Pulp (CIP) na Froth Floatation (FF) ambazo zimekuwa na tija zaidi kuliko matumizi ya zebaki ambayo imekuwa na athari nyingi za kiafya na mazingira sambamba na kiwango kidogo cha uzalishaji. 

Dkt. Biteko amesema kufuatia usimamizi thabiti na mabadiliko makubwa ya teknolojia ambayo kwa kiasi kikubwa yamechangiwa na uwepo wa maonesho hayo ya teknolojia, Serikali kupitia Wizara ya Madini imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi trilioni 3.8 kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025.

Akizungumzia hatua mbalimballi za Serikali katika kuhamasisha uongezaji thamani madini, Dkt. Biteko amesema kumekuwepo na uanzishwaji wa viwanda vya uyeyushaji na usafishaji wa madini ya dhahabu, nikeli na shaba katika maeneo mbalimbali nchini ambapo kwa sasa kuna jumla ya viwanda nane vya uchenjuaji wa shaba na nickel katika Mkoa wa Dodoma, Kiwanda kimoja cha Uyeyushaji wa Shaba (Chunya) na Viwanda Sita vya Usafishaji wa Dhahabu katika Mikoa ya Geita, Mwanza na Shinyanga-Kahama.

“ Nitoe wito kwa wachimbaji na Wizara kuendelea kubuni na kuongeza uwezeshwaji wa Watanzania kuongeza thamani ya madini wanayozalisha. Mazingira haya yataongeza upatikanaji wa fedha za kigeni pamoja na kuwapatia watanzania ajira kwenye viwanda vya uongezaji thamani, STAMICO mmefanya kazi kubwa sana kubadilisha na kushiriki kwenye local content.” Amesisitiza Dkt. Biteko.

Amewahakikishia kuwa Serikali sikivu inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya madini ikiwemo kufikisha huduma ya umeme katika maeneo yote muhimu.

Fauka ya hayo, Dkt. Biteko amewaasa washiriki wa maonesho hayo kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kwa kuwa hatua hiyo ni muhimu katika nchi ya kidemokrasia.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigella amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya ambapo mwaka jana aliagiza uwanja huo wa maonesho ujengewe miundombinu ya kudumu.

Amesema agizo hilo limetekelezwa na sasa uwanja huo una mabanda tisa ya kudumu ikiwa ni awamu ya kwanza ya ujenzi.

Amesema maonesho hayo kwa mwaka huu yamehudhuriwa na washiriki 930 wakiwemo washiriki kutoka nje ya nchi ikilinganishwa na washiriki 600 mwaka 2024.

Amesema “Rais Samia amewezesha kutoa leseni 9,000 kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wa Pori la Kigosi na sasa tumeweza kuzalisha zaidi ya tani 22,000 za madini kwa wachimbaji wadogo,” 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhandisi Zena Said amewashauri wadau wa sekta ya madini kwa ujumla kutumia fursa za taasisi za fedha ili kupata elimu kuhusu masuala ya fedha na uwekezaji.

Akimwakilisha Waziri wa Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo amesema maonesho hayo yamekuwa na manufaa mbalimbali ikiwemo kuwa chachu hususan kwa wachimbaji wadogo na kuwaongezea elimu kuhusu uchimbaji hatarishi na matumizi ya zebaki.

Vilevile amesema Wizara ya Madini itahakikisha inasimamia sheria na taratibu zote ili kufanya sekta hiyo kutoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo amesema kuwa hivi sasa sekta ya madini nchini imefikia kiwango cha kushawishi viwanda vya kuzalisha vipuri kuja kuwekeza Tanzania ili vipuri hivyo vipatikane nchini na kufikia lengo la kuwa na Tanzania ya viwanda.

Amebainisha kuwa Tume ya Madini itaendelea kuwezesha sekta ya madini ili kuhakikisha madini yanawanufaisha Watanzania wote.

Mwenyekiti wa Wachimbaji Wadogo, Lenard Bugomola amesema kuwa Mkoa wa Geita umekuwa ukiongoza kwa uzalishaji wa dhahabu, aidha ameomba STAMICO iwapatie mitambo miwili ya uchimbaji madini.

Awali Dkt. Biteko alitembelea mabanda ya mbalimbali yakiwemo Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini, Anglo Gold Ashanti, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Chama cha Wanawake Wachimbaji Madini Tanzania (TAWOMA), Mwamba Mining ambapo alielezwa kuhusu teknolojia ya kisasa ya uchimbaji madini

WASTAAFU KUPATA HUDUMA MAALUM ZA KIBENKI NA BIMA


Baadhi ya wastaafu na wataalam wa kifedha wakimsikiliza Meneja Mwandamizi wa Mauzo wa Benki ya Stanbic, Priscus Kavishe kwenye kongamano la wastaafu lililoandaliwa na Benki ya Stanbic Tanzania lenye lengo la kutoa huduma za kifedha na bima kwa wastaafu nchini. Kongamano hilo lilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.


…………….

Dar es Salaam, Septemba 26, 2025 – Wastaafu na wale wanaokaribia kustaafu nchini Tanzania wamehimizwa kujikita katika mipango thabiti ya kifedha, huduma za bima na uwekezaji ili kujihakikishia maisha yenye heshima na ustawi baada ya kumaliza muda wao wa kazi.

Ujumbe huu ulikuwa lengo kuu la Mkutano wa Wastaafu ulioandaliwa na Benki ya Stanbic, ambao uliwakutanisha wastaafu, wataalam wa kifedha na wadau wa sekta mbalimbali kujadili mbinu kwa vitendo ili kujiandaa kimaisha baada ya kustaafu. Tukio hili ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya Stanbic nchini Tanzania, yenye kaulimbiu ‘Miaka 30 ya Kukua Pamoja.’

Mjadala ulijikita zaidi katika akaunti ya Hekima Banking, akaunti maalumu iliyoanzishwa na Stanbic kwa ajili ya watu wenye umri wa miaka 55 na kuendelea. Akaunti hii inawapa wastaafu urahisi wa kufanya miamala, kuweka akiba, kupata mikopo na ushauri wa kifedha na uwekezaji.

Kwa mujibu wa Priscus Kavishe, Meneja Mwandamizi wa Mauzo wa Benki ya Stanbic, mpango huu umetengenezwa ili kuwapa wastaafu usalama na fursa. “Kwa Stanbic Bank, tunaamini kustaafu si mwisho, bali ni mwanzo wa fursa mpya. Kupitia Hekima Banking, tunawapa wastaafu suluhisho za vitendo zitakazowawezesha kuishi kwa heshima, kuwekeza na kuendelea kuchangia kwa maana katika familia na jamii zao,” alisema Kavishe.

Akaunti ya Hekima haina ada za kila mwezi, haina salio la chini, inapatikana kwa sarafu mbalimbali, na inatoa huduma za kidigitali saa 24/7. Wastaafu pia wanaweza kupata mikopo hadi TZS milioni 80 kwa masharti nafuu, huku mafao ya pensheni yakitumika kama dhamana. Aidha, wastaafu wanaweza kuomba bima ya afya pamoja na bidhaa nyingine za bima.

Umuhimu wa bima katika maisha ya kustaafu ulisisitizwa na Naphtal Ntangeki, Afisa wa Bima Stanbic, aliyebainisha kwamba bima ni nguzo muhimu ya mpango wa kifedha. “Kustaafu kwa usalama hakujengwi kwa akiba pekee. Bima inawapa wastaafu ujasiri wa kupanga maisha yao ya baadaye bila hofu ya misukosuko ya kifedha. Kwa Stanbic, tunaunganisha bima katika suluhu zetu ili wastaafu waweze kuishi miaka yao ya baadaye kwa uthabiti na heshima,” alisema Ntangeki.

Washiriki wa mkutano huo walipongeza hatua hii, wakibainisha kuwa imewapa maarifa na mbinu za moja kwa moja. Michael Liymbo kutoka KPMG, aliyeshiriki mkutano huo, alieleza tukio hilo kuwa na manufaa makubwa. “Mkutano wa leo umenifumbua macho. Nimejifunza jinsi akaunti ya Hekima Banking na huduma za bima zinavyoweza kusaidia wastaafu siyo tu kulinda fedha zao, bali pia kuishi maisha yenye heshima. Hatua hii ya Benki ya Stanbic kwa kweli inawanufaisha wataalamu na wastaafu wa baadaye,” alisema Liymbo.

Mkutano wa Wastaafu ni sehemu ya shughuli za mwaka mzima za Stanbic kuadhimisha miaka 30 ya shughuli zake nchini Tanzania. Zaidi ya kusherehekea historia yake, benki inatumia fursa hii kuanzisha suluhisho zinazooana na malengo ya Taifa ya Vision 2050 ya kukuza ujumuishaji wa kifedha, uthabiti na kuboresha maisha ya wananchi wote.

MWANAFUNZI APOKEA KITAMBULISHO CHA TAIFA, AISHUKURU NIDA





Careen Geofrey Erneo, mmoja wa wanafunzi wa Wilaya ya Ilala, ni miongoni mwa wananchi waliojitokeza katika Ofisi ya Usajili ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuchukua Vitambulisho vyao, mara baada ya kupokea ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) uliowataka kufika ofisini hapo mwishoni mwa wiki iliyopita.

Careen alieleza kuwa hatua hiyo ya kupata Kitambulisho chake kwa wakati ni jambo la kujivunia, kwani kitamrahisishia ushiriki wake katika shughuli mbalimbali za kijamii, kiuchumi na hata kielimu. Alisema kuwa Kitambulisho cha Taifa ni nyenzo muhimu kwa kijana wa kitanzania kwani ndicho kinachomtambulisha kisheria na kumfungulia fursa nyingi za kimaendeleo.

“Ninaishukuru sana NIDA kwa kuhakikisha napata Kitambulisho changu mapema. Hii imenipatia nafasi ya kuwa na uhakika katika masuala ya kitaaluma, kibenki na hata fursa za kijamii ambazo zinahitaji utambulisho rasmi. Kwa kweli, hii ni hatua kubwa kwangu kama kijana,” alisema Careen mara baada ya kukabidhiwa kitambulisho chake.

Aidha, aliwataka vijana wenzake, hususan wanafunzi, kujitokeza kuchukua vitambulisho vyao pale wanapopata taarifa kupitia SMS au tangazo lolote rasmi kutoka NIDA. Alisema kitambulisho hicho si tu kinahitajika kwa ajili ya shughuli za kila siku, bali pia ni nyenzo muhimu katika kujenga mustakabali wa maisha yao.

“Vijana wenzangu ambao bado hawajasajiliwa, nawahimiza wajitokeze kwa wingi ili wapate haki yao hii ya msingi. Kitambulisho cha Taifa ni cheti cha uraia wetu na ni sehemu ya msingi wa maendeleo yetu binafsi na ya taifa kwa ujumla,” alisisitiza.

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa sasa inaendelea na jitihada za kuhakikisha wananchi wote wenye sifa wanapata Vitambulisho vyao, ikiwa ni pamoja na kuwasilisha SMS kwa wananchi walio tayari kukabidhiwa vitambulisho vyao, ili kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa huduma na kupunguza msongamano katika ofisi zake.

TANAPA YASHIRIKI MAPOKEZI YA MWANARIADHA BINGWA WA DUNIA SAJINI TAJI SIMBU - ARUSHA.










Na. Jacob Kasiri - Arusha

Leo Septemba 29, 2025 TANAPA imeshiriki hafla ya mapokezi ya Bingwa wa Dunia mbio ndefu (Marathon) kilometa 42  Sajini Taji Alphonce Simbu yaliyofanyika  takribani wiki mbili jijini Tokyo - Japan, mapokezi yaliyofanyika katika Uwanja wa Ndege Kisongo jijini Arusha.

Katika mapokezi yaliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), SGT Simbu aliwashukuru TANAPA kwa kushiriki mapokezi hayo na kumuandalia gari alilotumia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa maandalizi ya filamu ya “Tanzania:The Royal Tour”.

Simbu aliongeza kuwa licha ya heshima aliyoipata duniani ya kushinda medali ya Dhahabu katika mbio hizo za km 42, pia TANAPA imempa heshima isiyo kifani kutumia gari aliyotumia Mkuu wa nchi kama filamu yake iliyojizolea umaarufu ndani na nje ya Taifa letu.

Wakati wa kuhitimisha hafla ya mapokezi hayo yaliyofanyika katika uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

UTAFITI MIAMBA BONDE LA EYASI WEMBERE WATHIBITISHA UWEZEKANO WA UPATIKANAJI MAFUTA

📌 *Dkt Mataragio akagua shughuli za utafiti na kutoa maelekezo kwa TPDC/AGS*  📌 *Awamu ya  pili ya utafiti kukamilika Aprili 2026.*   *📌A...