Sunday, September 17, 2017

WAFANYAKAZI 17 WA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA WA NCHINI UGANDA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA NCHINI (CATC).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari akizungum za katika mahafali 270 ya Chuo cha Usafiri wa Anga CATC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA),jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Usafri wa Anga (CATC), Dk. Daniel Karenge akitoa taarifa ya Chuo hicho katika mahafali ya 270 yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga(TCAA), jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari akitoa cheti kwa Mhitimu wa Kozi ya Watoa Taarifa za Usafiri wa Anga, Stella Kabagenyi katika mahafali ya Mahafali ya 270 ya Chuo cha UsafiriwaAnga Tanzania(CATC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.
Sehemu ya wahitimu wakionesha vyeti vyao katika mahafali ya 270 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari akiwa katika picha pamoja na wahitimu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) katika mahafali ya 270 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.
Na ChalilaKibuda, GlobuyaJamii

WAFANYAKAZI 17 wa Mamlaka ya Usafiriwa Anga wa Nchini Uganda wamehitimu mafunzo katika kozi mbalimbali katika Chuo cha Mamalaka ya Usafiri wa Anga wa nchini (CATC).

Akizungumza katika mahafali ya 270 ya Chuo hicho ,MkurugenziMkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari amesema kuwa waliohitimu mafunzo katika chuo hicho wakatumie elimu ambayo italeta mabadiliko katika usafiri wa anga.

Amesema chuo cha CATC kinatambulika na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) hivyo mafunzo yanayotolewa ni bora kutokana nakutambulika kwa nchi mbalimbali kuleta watalaamu wao kuja kujifunza masuala ya usafiri anga nchini Tanzania.

Hamza amesema tofauti kinachofanya kwa watalaam hao kuwa wameiva ni kuonyesha mikakati yauekelezaji kwa kile walichojifunza katika maendeleo ya nchi yao pamoja na Afrika Mashariki katika utoaji wa huduma ya usafiri wa anga.

Amesema mikakati iliyopo kwa chuo hicho ni kuingia ubia na Chuo cha Nchini Singapore kwa ajili ya kutoa mafunzo ya usafiri wa anga kwa nchi za Afrika hali ambayo itafanya Chuo kuongeza idadi ya wanafunzi wanakuja kusoma na kuifanya Tanzania kutambulika zaidi katika utoaji wamafunzo ya usafiri wa anga.

Nae Mkuu wa Chuo CATC, Dk. Daniel Karenge amesema kuwa wahitimu waliohitimu chuo hicho tangu kilipoanzishwa mwaka 2000 niwahitimu 3056 katoka nchi mbalimbali zaAfrika .

Amesema kuwa wanaopata mafunzo hayo kwa asilimia kubwa ni watu wa nje ya nchi hivyo amewasaa watanzania kutumia fursa ya kupata mafunzo ya usafiri wa anga katika chuo chao.

No comments: