Thursday, September 27, 2012

Majina ya makada wa CCM walioteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongoz

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), jana kimetangaza majina ya makada wake walioteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi, ambapo vijana wameonekana kupewa nafasi kubwa zaidi za kuwania fursa ya kukiongoza Chama hicho kikongwe nchini.
Vijana wengi wameonekana kuchomoza katika nafasi za uenyekiti, makamu mwenyekiti, itikadi na uenezi, uchumi na fedha na zile za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC).
Miongoni mwa vijana mahiri na wenye uwezo mkubwa katika uongozi walipata fursa ya kupitishwa na NEC ni pamoja na Paulo Herman Kirigini, ambaye ameteuliwa kuwania ujumbe wa NEC kupitia viti vitatu bara kwa kundi la Wazazi, ambako atachuana na wakongwe kadhaa wakiwemo mawaziri na wabunge.
Vijana wengine waliochomoza katika kuwania nafasi mbalimbali ni Christopher Pallangyo (Mwenyekiti wilaya ya Meru), Latifa Ganzel (Morogoro Mjini), Harold Lyimo (Arusha), Peter Mushao (Longido), Nanai Konina (NEC- Monduli), Patrick Myovela (Iringa Vijijini), Muhaji  Bushako, Alice Mjula (Muleba) na Asad Salum Kikule (Kilolo).
Wengine ni Murdhid Ngeze (Bukoba Vijijini), Revocatus Babeiya, Editha Kokutona Rwezaula, Alistides Mujwahusi, Lucas Zakaria, Janes  Darabe.
Vijana wengine ni Dk. Sebastian Ndege (NEC-K-ndoni), Thabiti Ntuyabaliwe (NEC-Kndoni), Saidi Omar (NEC-K-ndoni).
Wengine ni Issa Mangungu (31) Phares Magesa (33) NEC Temeke,  Leonard Bugomola (27),
Malugu Mwendesha (33) nafasi ya katibu uchumi mkoa wa Geita, Christian Sinkonde (31) NEC Kisarawe.
Vijana wengine waliochomoza kwenye nafasi ya NEC, Morogoro Vijijini Omari Mgumba (36)
Robert Selasela (28), Zuberi Mfaume (39) na Morogoro Mjini ni Robert  Makorere (32),Kelvin Mutatila Njuwa (33 na Amina  Mhina (36).
Kuteuliwa kwa idadi kubwa ya vijana kunaashiria kuwa CCM imeanza kutekeleza mikakati yake ya kuendelea kukisuka upya na kuingiza damu changa kwa ajili ya kuendeleza mapambano ya kisiasa na kuwadhibiti wapinzani.

No comments: