Thursday, September 27, 2012

Bendi mbalimbali kukamua kukamua tamasha la Tanzania Live Music Festival kesho Leaders


 
Balozi wa tamasha la Tanzania Live Music Festival Jackline Wolper akizungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Leaders leo wakati wandaaji wa tamasha hilo walipozungunzia kukamilika kwa maadalizi  katika picha wanaofuatia ni Mzee King Kikii, Tarsis Masela  wa Akudo Impact na Jamwaka kutoka Sikinde
……………………………………….
Tanzania Live Music Festival imewadia! ambapo kuanzia kesho tarehe 28/29 mashabiki wote wa muziki wa dansi jijini  Dar es saalam wanakaribishwa kuburudika na muziki wa wa dansi bila kikomo,katika viwanja vya Leaders jijini  ikijumuisha bendi zaidi ya kumi ambazo zitakuwa zikiimba live.
Bendi zitakazo tumbuiza ni Sikinde, Msondo, B Band Mashujaa Band, Akudo, FM Academia, Wazee Sugu na wengine kibao!
Lakini pia kutakuwa na bendi zitakazosindikiza onesho hilo  kama vile Khadija Kopa malikia wa Mipasho na Mashauzi Classic chini ya Isha Mashauzi.
Lengo kubwa la Tamasha hili ni kusaidia Chama cha Dansi Tanzania CHAMUDATA ili kuboresha na kuendeleza chama hicho.
waandaajiwa tamasha hilo wametoa shukurani kwa  Kampuni zote ambazo zimekuwa zikiunga mkono maadalizi yote  ili kufanikisha  Tamasha hili.
Kampuni hizo ni
TIMES FM, GLOBAL PUBLISHERS, MAJIRA, WHINDHOEK, REAL STAR, FLY 540, FACE TO FACE BAR and RESTAURANT, PUSH MOBILE
Wapenzi wote wa muziki wa dansi mnakaribishwa kujiunga pamoja na kupata burudani. Kiingilio ni 20,000 kwa VIP na 5000 kwa tiketi za kawaida. Wote mnakaribishwa.

No comments: