Monday, January 23, 2017

NITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI KULETA MAENDELEO-KUMBILAMOTO

Naibu Meya wa Manispa aya Ilala, Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kikundi cha Makazi Kazi kilichopo katika mtaa wa Kaza Buti
 
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala akizungumza na Wananchi wa eneo la mtaa wa Kaza Butu katika kata ya Vingunguti.

 
Mwenyekiti wa Haki za Binadamu wa Chama cha Wananchi (CUF) Mohamed Mluya, Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara
Mjumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) Salma Emmanuel, Akizungumza juu ya mambo yake yaliyotekelezwa na Diwanihuyo
Mwenyekiti wa Haki za Binadamu wa Chama cha Wananchi (CUF) Mohamed Mluya, akikabidhi jezi kwa vikundi vya Joging
Naibu Meya na wenzie wakicheza muziki mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo
Wananchi wakifatilia mkutano huo kwa makini
Baadhi ya vijana wa mtaa wa kaza buti wakifatilia kwa makini mkutano huo unavyoendelea
Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mtambani ,Sharifu Abdalah akikabidhi jezi kwa kikundi cha Joging
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala akisalimiana na wazee maharufu mara baada ya kumalizika kwa mkutano wake na wananchi wa mtaa wa Kaza buti
Dj akifanya yake katika mkutano huo.

Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii 


Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vinguti , Omary Kumbilamoto, ameahidi kuendelea kushirikiana na wakazi wa kata hiyo hili kuakikisha wanapata maendeleo. 

Kumbilamoto amesema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa mtaa wa Kaza buti kata ya Vingunguti wakati akikabidhi vifaa vya michezo na mabati kwa tasisi ya Makazi kazi na vikundi vya michezo. 

“nitoe shukrani kwa wakazi wa eneo la kazabuti kwa jinsi mlivyoweza kuniamini katika uchaguzi mkuu mwaka jana na kunipa fursa ya kuwa Diwani wenu na leo nimekuja kuwatembelea kwa ajili ya kutimiza moja ya ahadi zangu hivyo naomba niwaambie kuwa nitakuwa nanyi bega kwa bega katika kuakikisha kuwa tunaleta maendeleo katika kata yetu” amesema Kumbilamoto. 

Kumbilamoto amesema kuwa amemaliza mwaka mmoja ndani ya utawala wake kwa kuweza kutimiza ahadi kadhaa ambazo aliahidi ikiwemo ununuzi gari ya kubebea wagonjwa , Mashine yakufulia katika Zahanati ya vingunguti na ujenzi wa choo kwa ajili ya wodi ya kinamama wajawazito. Aidha ametaja kuwa pia katika mwaka huu mmoja maeweza kuwasaidia wanawake wajasilimali ambao aliwapa vyerehani viwili hiki kuendeleza vikundi vyao. 

Kumbilamoto alimaliza kwa kuwataka wakazi wa Vingunguti kuwa wachapakazi kwa kila jambo kama Rais wanchi Dkt John Pombe Magufuli.

No comments: