Tuesday, October 19, 2010

Mwenyekiti wa wazee ajisalimisha



Mwenyekiti wa wazee waliokua wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Nathaniel Mlaki akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam baada ya kujisalimisha katika ofisi ya kamanda wa Kanda maalum, Suleiman Kova (kulia). Ndugu Mlaki alitakiwa kujisalimisha baada ya kutoa taarifa za uongo kwenye vyombo vya habari za kufa kwa mzee mwenzao, Anderson Msuta wakati wazee hao walipofunga barabara ya kivukoni na kuondolewa na polisi. Mzee Msuta alijitokeza juzi na kukanusha uvumi wa kufa kwake.( Picha Na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi).

No comments: