Sunday, October 24, 2010

Mashabiki saba wafariki uwanjani Nairobi



Mashabiki saba wamekufa katika uwanja wa soka wa Nyayo, mjini Nairobi, kufuatia mkanyagano katika uwanja wa Nyayo.

Habari za awali zilikinukuu kituo cha matangazo cha Jambo FM.

Hayo yalitokea katika mechi ya ligi kuu ya Kenya, kati ya timu za Gor Mahia na AFC Leopards.
Kulingana na kituo hicho ambacho kwa kawaida hutangaza moja kwa moja mechi za soka, watu hao saba walikufa baada ya mashabiki kujaribu kuingia uwanjani kwa kutumia mabavu, ili kutizama mechi hiyo ya vilabu hivyo vikongwe, ambavyo ni kati ya vilabu maarufu zaidi vya soka nchini Kenya.

Kituo cha matangazo cha Jambo FM kilielezea kwamba licha ya vifo hivyo vya mashabiki hao saba kutokea, mwamuzi hakusitisha mechi hiyo. Mechi hiyo pia ilichezwa katika mazingira ya mvua kubwa.

Habari kwa hisani ya www.bbcswahili.com

No comments:

DKT. ABBASI AKAGUA MIRADI YA UTALII PORI LA AKIBA LA PANDE, ATOA MAAGIZO YA KUKAMILIKA KABLA YA AFCON 2027

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, leo Julai 23, 2026, ametembelea Pori la Akiba la Pande jijini Dar es Salaa...