Saturday, October 23, 2010

Breaking Newzzz Dk Slaa: Huwezi kumtaja rais kwenye ufisadi ukawa salama


Nimemsikiliza live Dk Slaa katika mdahalo wake uliomalizika muda mfupi uliyopita, miongoni mwa aliyoyasema ni haya, "Huwezi mtaja raisi kuwa ni fisadi lakini bado unaishi!!!! sibaatishi!!! kunywa chai na Obama halafu hamna hela.



Nyingine amesema kama urais ni kumwaga damu hautaki, na kwamba akasema “mtu akikupiga kofi mgeuzie, wametuchafua mnooo... ukiona refarii anasema mpira ukiisha matokeo ni draww ogopa


‎" Siyo TRA peke yake uchafu uko kila kona nikiingia madarakani sitakuwa na msamaha na mtu, nimewaambia huko katika kampeni, warudishe fedha walizoiba...nimepita pale muheza nikaambiwa kuna nyumba ya dk wa wilaya imejengwa kwa milioni 70, ukiangalia ni aibu wananchi wakaja kwenye gari yangu wakaninong'oneza wakasema hiyo nyumba tumejenga sisi kwa michango yetu , imekamatwa mifugo yetu.. fedha kumbe zimeliwa huu ni mfano wa wizi uliopo kila kona,"Dk Slaa anasisitiza


‎"Tuna taarifa mabango yaliyobandikwa kote nchini na hata katika nyumba mbovu za nyasi huko vijijini nimepita nimeshuhudia nyumba zinataka kuanguka lakini zina mabango ya bure, mabango haya yametengenezwa Canada kwa gharama ya dola zaidi ya milioni moja, na yalipofika hapa nchini hayakulipiwa kodi, halafu CCM wanasema hawawezi kusomesha watoto bure huuu ni ufisadi!!!,"Dk Slaaa ananena!




No comments: