Saturday, June 16, 2007

Tuesday, June 12, 2007

Kwa mtaji huu, tunaelekea kwenye utawala wa kifalme-2

NIMELAZIMIKA kuendeleza mjadala huu kutokana na mwitikio mkubwa wa wasomaji wetu wa safu hii ya siasa. Wiki iliyopita, nilizungumzia kwa kina kuhusu namna ambavyo watoto wa maskini na au maskini wenyewe wazazi au wao walivyo na fursa ndogo ya kuweza kupata madaraka katika chama na au serikali.

Nimefurahi kwamba wapo wengi ambao walikuwa na mtazamo kama wangu, yaani wa kupinga mifumo inayowafanya nafasi watoto wa vigogo na watu wengine wenye uwezo kuwa na uwezekano mkubwa wa kunyakua madaraka ya uongozi kwa hali yoyote ile na hivyo kuwanyima fursa wale wasio nacho hata kama wana uzoefu au uwezo mkubwa.

Nimefurahi, pia kwamba wapo watu wengine wenye mitazamo inayoafiki kwamba wao ndiyo wao, ndio wateule na kwamba eti kwa sababu watoto wao wamezaliwa katika siasa, basi wataendelea kuwa wafalme wa siasa, daima dawamu hadi dunia hii inakwisha.

Sunday, June 03, 2007

Mpango wa njia tatu Dar ufutwe, haufai



Barabara ya Morogoro.

WIKI hii tumeshuhudia utekelezwaji wa maamuzi makubwa na ya haraka haraka mno ambayo kwa upande mmoja yanaweza kuonekana kama ni ukombozi kwa watu wengine, lakini kwa upande mwingine ni kero na tatizo kubwa zaidi kwa raia wa taifa hili walioko jijini Dar es Salaam.

Hii inafuatia utekelezwaji wa amri ya Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliyetaka kumalizwa kwa tatizo la msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na hivyo kuchukuliwa maamuzi ya haraka haraka ya kuanza kutumika kwa njia nyingine ya ziada kwa magari yanayokwenda na au kurudi mjini wakati wa asubuhi na jioni.

Sikatai kwamba ili kifanyike kitu kikubwa, ni lazima kufanya maamuzi magumu, lakini kwa mantiki ya sasa uamuzi huu mgumu hauna manufaa makubwa kuliko hasara zilizopo. hapa

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AMPONGEZA NDEJEMBI, AMSIFIA KWA UADILIFU NA UCHAPAKAZI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba , amempongeza Mhe. Deogratius John Ndejembi kwa kuaminiwa ...