Sunday, June 03, 2007

Mpango wa njia tatu Dar ufutwe, haufai



Barabara ya Morogoro.

WIKI hii tumeshuhudia utekelezwaji wa maamuzi makubwa na ya haraka haraka mno ambayo kwa upande mmoja yanaweza kuonekana kama ni ukombozi kwa watu wengine, lakini kwa upande mwingine ni kero na tatizo kubwa zaidi kwa raia wa taifa hili walioko jijini Dar es Salaam.

Hii inafuatia utekelezwaji wa amri ya Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliyetaka kumalizwa kwa tatizo la msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na hivyo kuchukuliwa maamuzi ya haraka haraka ya kuanza kutumika kwa njia nyingine ya ziada kwa magari yanayokwenda na au kurudi mjini wakati wa asubuhi na jioni.

Sikatai kwamba ili kifanyike kitu kikubwa, ni lazima kufanya maamuzi magumu, lakini kwa mantiki ya sasa uamuzi huu mgumu hauna manufaa makubwa kuliko hasara zilizopo. hapa

No comments: