Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, leo tarehe 3 Agosti 2026 amewasili katika Viwanja vya John Malecela jijini Dodoma, yanakofanyika Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane 2026.
Baada ya kuwasili, Mhe. Dkt. Nchimbi ametembelea mabanda mbalimbali na kujionea teknolojia, tafiti, bidhaa na huduma zinazotolewa na taasisi pamoja na wadau wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.
Makamu wa Rais ni mgeni rasmi katika Siku Maalum ya Ushirika na Maadhimisho ya Miaka 10 ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), yanayofanyika leo ndani ya Maonesho hayo.
Ushiriki wake unaendelea kusisitiza dhamira ya Serikali ya kuimarisha ushirika, utafiti, matumizi ya teknolojia na ubunifu ili kuongeza tija na kuharakisha maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.
#Nanenane2026 #Dodoma #Ushirika #TARI #KilimoChaKisasa







No comments:
Post a Comment