Thursday, December 18, 2008

Herry Makange afariki dunia




HAYATI HERRY MAKANGE

Habari tza kusikitisha tulizozipoke hivi punde kutoka kwa issamichuzi.blogspot.com zinasema kuwa HERRY MAKANGE, MPIGANAJI WA CHANNEL TEN NA DTV, HATUNAYE TENA BAADA YA KUFARIKI KATIKA AJALI HAPA DAR JANA MCHANA.

HABARI ZILIZOPATIKANA JANA USIKU NA KUTHIBITISHWA ASUBUHI HII NI KWAMBA HERRY ALIKUTWA NA MAUTI AKIELEKEA MJINI KUTOKEA KAWO KIBAHA AKIWA ANAENDESHA PIKIPIKI. ALIKUWA NDIO KWANZA AMEREJEA TOKA TABORA KIKAZI NA ALIKUWA AKIENDA KURIPOTI KAZINI.
IKUMBUKWE KWAMBA HERRY ALIKUWA MMOJA WA WAPIGANAJI WALIONUSURIKA KATIKA AJALI YA GARI HUKO KIBITI ILIYOMHUSISHA PIA MPIGANAJI ATHUMANI HAMISI AMBAYE HADI LEO YUKO SAUZI AKITIBIWA SHINGO NA MGONGO. KURASA YA AJALI HIYO YA KIBITI BOFYA HAPA
TUTAENDELEA KUFAHAMISHANA KILA KINACHOJIRI BAADAYE IKIWA NI OAMOJA NA MIPANGO YA MAZISHI.
MUNGU AILAZE ROHO YA MPIGANAJI MWENZETU MAHALI PEMA PEPONI
-AMINA

1 comment:

Anonymous said...

Poleni sana famlia ya Bwana Makange, Bwana alito na Bwana ametwaa jinalake lihimidiwe. Nampa pole san mke wake mpenzi ambaye ni mwezi uliopita tu walifunga ndoa, leo hii mwenyezi mungu amewatenganisha, pole sana dada.
Raha ya Milele Umpe Ee Bwana na Mwanga Wa Milee Umwangazie, Apumzike kwa Amani.AMEN.

Msomaji wa blog.