Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, ameipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchukuzi (NCT) uliofanyika katika Ukumbi wa Gallagher Estate jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mkutano huo uliofunguliwa na Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, uliwakutanisha viongozi wa sekta ya uchukuzi kujadili mustakabali wa mifumo jumuishi, salama na endelevu ya uchukuzi barani Afrika.
Katika mjadala wa Mawaziri wa Uchukuzi, Kihenzile aliwasilisha mafanikio makubwa ya Tanzania, akibainisha uwekezaji unaoendelea katika miradi ya kimkakati ikiwemo reli ya kisasa ya SGR, maboresho ya bandari, viwanja vya ndege pamoja na miundombinu ya barabara.
Aidha, alisisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania katika kuimarisha mazingira rafiki kwa uwekezaji, akiwakaribisha wawekezaji wa ndani na nje kushiriki katika miradi ya uchukuzi yenye lengo la kukuza biashara, ajira na maendeleo ya kijamii katika ukanda wa Kusini mwa Afrika.
#Tanzania #Transport #SGR #Investment #Africa #Infrastructure #EconomicGrowth #Johannesburg #NCT #Development









.jpeg)
No comments:
Post a Comment