Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa kwa kushiriki kikao muhimu cha Baraza la Uongozi la Umoja wa Afrika (African Union Bureau of Assembly), kilichofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 26 Machi 2026.
Kikao hicho kilichofanyika kutoka Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar, kiliwakutanisha viongozi wakuu wa Bara la Afrika kujadili masuala ya kimkakati yanayolenga kuimarisha mshikamano, kukuza uchumi na kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi wa Afrika.
Mheshimiwa Dkt. Samia, ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), alishiriki kikamilifu katika majadiliano hayo, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda na maendeleo jumuishi.
Mkutano huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Rais wa Jamhuri ya Burundi Mheshimiwa Évariste Ndayishimiye, ambapo ajenda kuu zilihusu kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuimarisha amani na usalama, pamoja na kukuza uchumi wa bara kwa manufaa ya wote.
Ushiriki wa Mheshimiwa Dkt. Samia unaendelea kudhihirisha dhamira ya Tanzania ya kuwa sehemu muhimu ya ujenzi wa Afrika yenye umoja, nguvu na ustawi wa pamoja.
#SamiaSuluhuHassan #Tanzania #AfricanUnion #AU #Diplomasia #Uongozi #Maendeleo #Afrika #Ushirikiano #GlobalLeadership

.jpeg)

No comments:
Post a Comment