Sunday, December 12, 2010

KILIMANJARO STARS MABINGWA WAPYA WA CECAFA


Timu ya Taifa Stars imenyakua ubingwa wa kombe la Tusker Cecafa, Challenge Cup baada ya kuibwaga Ivory Coast kwa bao moja kwa bila katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo iliyomalizika muda mfupi uliopita katika uwanja wa taifa.

Mfungaji wa bao hilo alikuwa nahodha wa timu hiyo ya taifa Shadrack Nsajigwa kwa njia ya penati ambapo alikung’uta mkwaju mkali ulioingia wavuni na kumwacha kipa wa timu ya Ivory Coast akigaragara, hiyo ilikuwa dakika ya 31.

Mara baada ya kufunga bao hilo uwanja uliripuka kwa furaha na vifijo, Ushindi huo umekuwa zawadi kuu kwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, Maalim Seifa Shariff Hamad. Mshindi wa tatu ni timu ya Uganda ambayo imemrambisha Ethiopia bao 4-3.

No comments:

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AMTEMBELEA MHE. FARIDA AMOUR MOH'D HOSPITALINI, AMTAKIA AFYA NJEMA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla , leo tarehe 21 Mei 2026 amemtembelea na kumjulia hali Mwakilishi wa Viti M...