Sunday, June 03, 2007

Kwa mtaji huu, tunaelekea kurudi kwenye utawala wa kifalme



Mmoja wa watoto wa Vigogo akikabidhiwa fomu.

HATA kama hatutaki, basi hivi ndiyo ilivyo, pia ndivyo ilivyojengwa ikafanyiwa mikakati ya makusudi na kama haikemewi haitabadilika, tunaelekea kunako utawala wa familia, utawala wa kifalme wa baba kumwachia mwana na mwana, mke na hadi mjukuu au mkwe na mzunguko unabakia kuwa ule ule.
<>

Sasa hivi ni wakati wa mchakato wa wanachama kuomba kuteuliwa kuwa viongozi ndani ya chama tawala, kile cha Mapinduzi, CCM, hasa kwa ngazi ya ujumbe wa halmashauri kuu na hatimaye kamati kuu, ngazi ambazo ni nyeti ndani ya chama hicho.
Kutokana na mchakato huo, wiki iliyopita tumeshuhudia watoto wa vigogo, wake zao, wajukuu na hata babu zao wakifurukuta na kuchukua fomu hizo kwa nia au lengo la kubakia katika madaraka ya ngazi za juu ndani CCM. Hawa wanajidanganya kama vile kwamba baba akiwa na kipaji basi na mwana anacho. La hasha kila mtu na kipaji chake kwa maana hiyo siyo kweli kwamba kila mtoto wa kigogo ana kipawa na au uwezo wa kuongoza. Uongozi siyo inherent. Bonyeza hapa kuendelea kujipatia uhondo.

No comments: