Wednesday, June 27, 2007

Buriani Amina Chifupa



Mheshimiwa Amina Chifupa hatunaye tena, kwa mujibu wa baba yake Amina, Mzee Hamis Chifupa, bintiye alikutwa na mauti saa tatu kasorobo usiku katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo alikokuwa amelazwa. Kifo chake kimepokelewa kwa hisia mbalimbali na watu wa rika tofauti nchi nzima.



Medy Mpakanjia analia.



Gari iliyobeba mwili wa Amina.



Kwaheri Amina Picha hii imepigwa na Mpoki Bukuku.

RATIBA YA MAZISHI ILIYOPATIKANA NYUMBANI KWA MZEE CHIFUPA
MIKOCHENI ENEO LA TPDC ZINASEMA...

Mazishi yatafanyika Kesho, Kijijini Kwao Luhanjo, Lupembe, Njombe Mkoani Iringa, Ngugu, jamaa na Marafiki wanaotaka kuhudhuria Mazishi hayo kutoka Dar es salaam Wanatakiwa Kutoa Mchango wa Tshs 40,000/= Ili waondoke kwa Msafara wa Pamoja! Dk. Tamba ndo Mweka hazina wa kamati ya Mazishi na ndo anapokea Michango hiyo ya tshs. 40,000/= kwa Kila mmoja kama nauli ya kwenda na Kurudi Mazishini!

Taarifa hizi kwa mujibu wa Ngowi au Michuziutapata taarifa za kina.

Mola ailaze pema Roho ya Mpendwa wetu Amina Chifupa- Amina.

No comments: