Sunday, February 27, 2011

Ajali yaua Watano



WATU watano wamekufa papo hapo na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ilihoyahusisha magari mawili ya abiria yanayofanya safari zake kati ya Kahama na Dar-Es-Salaam na jingine Itigi –Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa sita mchana eneo la Mbwanga karibu na mizani ya Tanroad ,nje kidogo ya mji wa Dodoma ilihusisha basi la kampuni Ally`s lenye namba T312 AUU lililokuwa likitokea Kahama kuelekea Dar-Es-Salaam ambapo liligongana na gari aina ya Coaster leny namba T896BGH ambalo lilikuwa likitokea Dodoma kuelekea Itigi wilayani Manyoni .

Kwa mujibu wa miongoni wa majeruhi wa ajali hiyo,chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa basi dogo ambaye alitaka kulipita gari jingine huku akiwa katika mwendo mkali.

Walisema alipokuwa akitaka kulipita gari jingine huku akiwa katika mwendo mkali,ghafla alikutana na gari jingine hivyo akaamua kukatisha barabara jambo ambalo lilisababisha dereva wa basi kubwa(ally`s) kujikuta ameligonga basi dogo ubavuni.

No comments: