Sunday, February 20, 2011

Athari za mabomu





ZAIDI ya mabomu 1,360, miongoni yakiwemo makombora, yamekusanywa Maofisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ili kuondoa hatari ya kuwepo kwa milipuko mingine kwenye maweneo ya makazi ya watu.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), Luteni Kanali Kapambala Masoud Mgawe alisema kuwa, kazi hiyo imefanywa usiku kucha na askari hao ili kuzuia athari zilizojitokeza kwenye maeneo hayo.

Alisema, mpaka sasa askari hao bado wanaendelea na kazi hiyo kwenye maeneo tofauti yaliyoathirika na mabomu hayo.

“Askri bado wanaendelea na zoezi la kutafuta mabomu kwenye maeneo ya wananchi, hivyo basi tunawaomba watoe ushirikiano ikiwa ni pamoja

Aliongeza maeneo ambayo yameanza kufanyiwa kazi ni pamoja na Majohe, Gongo la Mboto karibu na kambi na Pugu, ambako ndiko kulikohathirika zaidi na mabomu hayo.

Alibainisha, kutokana na hali hiyo wananchi wasiwe na wasiwasi juu ya hali ya mabomu hayo kwa sababu askari wapo kwa ajili ya kulishughulikia suala hilo ili lisiweze kuwaathiri wananchi na mali zao.

Kwa mujibu wa Mgawe, wananchi wasichezee mabomu hayo kwenye maeneo hayo, kwa sababu wanaweza kusababisha hatari, hivyo basi wametakiwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika pindi wanapoyaona ili waweze kuyachukua.

No comments: