Thursday, November 06, 2008

Vurugu chuo kikuu




Unaona hapa ni kama vile kuna vita, wala si watu wengine bali ni wanafunzi wa Chuo KIkuu cha Dar es salaama wakipambana wao kwa wao ambapo wamewajeruhi wenzao kwa mawe na chupa katika harakati za kuwaondoa wengine madarasani.

Tukio hilo lilisababishwa na vurugu kati ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliogoma wakitaka wapewe asilimia 100 ya mikopo inayojumlisha fedha za kujikimu na ada za masomo na baadhi yao ambao walipinga mgomo huo, baada ya waliogoma kuwalazimisha wenzao kutoka madarasani.

Wanafunzi wawili wamelazwa katika zahanati ya chuo ambao ni Makala Simon mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo cha Uhandisi na Teknolojia ambaye amepigwa jiwe na kujeruhiwa shavu la kushoto.

Pia yupo Benedict Edward aliyejeruhiwa kichwani baada ya kupigwa chupa ya soda kichwani ambaye hali yake ilizidi kuwa mbaya na akapelekwa hospitali ya Misheni Mikocheni kwa matibabu zaidi.

1 comment:

Anonymous said...

MSAMA NI TAPELI WADAU HEBU FANYIENI KAZI HILI SWALA KWANI ANAAIBISHA NA KUIBA KUPITIA KIVULI CHA ULOKOLE. KATAPELI JAMAA WA UPANGA MILLIONI SABA.

KATAPELI TBC MILIONI NNE IKIWAPO CHEQUE FEKI NA SASA TBC KUMFIKISHA MAHAKAMANI NA KUMTANGAZA TBC ONE NA REDIONI KAMA TAPELI MLOKOLE FANYENI UTAFITI.