Wednesday, November 12, 2008

Chuo Kikuu watimuliwa









UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampasi ya Mlimani umewasimamisha masomo wanafunzi wa shahada za kwanza kwa muda usiojulikana.

Hatua hiyo imekuja baada ya wanafunzi hao kukaidi amri ya chuo pamoja na ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof Jumanne Maghembe, iliyowataka kusitisha mgomo na kurudi madarasani wakati wizara ikishughulikia madai yao.

Kufuatia hatua hiyo, Rais wa Serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, Anthony Machibya, aliwatangazia wanafunzi wenzake juu ya kusimamishwa huko na kusisitiza kuwa, pamoja na kufukuzwa chuoni hapo, lakini watakaporudi wataendeleza harakati za kudai haki yao mpaka watakapoipata.

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...