Wednesday, November 12, 2008

Uingereza yabana masharti ya viza

KWA wale wanaotaka kwenda Uingereza bila ya mipango ya muda mrefu, sasa wanatakiwa kujipanga upya; Uingereza imeongeza masharti mapya na magumu ya viza duniani kote.

Watanzania wanaokadiriwa kuwa kati ya 8,000 na 9,000 huomba visa ya kuingia taifa hilo kongwe kila mwaka, lakini masharti hayo mapya yanaweza kufanya idadi hiyo kupungua.

Moja ya masharti hayo ni lile linalomtaka Mtanzania yeyote anayetaka kuingia Uingereza, kama ilivyo kwa raia wengine wote wasio Waingereza duniani kote, sasa anapaswa kuwasilisha maombi ya viza wiki sita kabla ya siku ya safari.

"Ubalozi wa Uingereza hautakuwa tena na uwezo wa kuwezesha upatikanaji wa viza, ikiwa mwombaji atatoa taarifa ya muda mfupi," alisema afisa habari wa ubalozi wa Uingereza nchini, John Bradshaw.

No comments: