Tuesday, November 25, 2008

Mramba, Daniel Yona kizimbani kwa ufisadi







MAWAZIRI wawili waliowahi kuongoza wizara mbalimbali ikiwamo nyeti ya fedha katika serikali ya awamu tatu, Basil Mramba na Daniel Yona wamefikishwa kortini kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Mramba na Yona walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana mbele ya Hakimu Hezron Mwankenja saa 5.40, wakasomewa mashtaka na baadaye kupelekwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Vigogo hao walifikishwa mahakamani baada ya uvumi wa tukio hilo kudumu kwa takribani majuma mawili.

Wakati wakiingia mahakamani jana Mramba ambaye ni mtuhumiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 1200 ya mwaka huu, alisikika akiwahoji waandishi iwapo wamefurahi kufikishwa kwao mahakanai hapo, huku akidai kuwa watapiga picha

No comments:

TRENI YA MWENDOKASI KUFIKA MWANZA 2028

  Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kulia),akizungumza baada ya kukagua daraja la kupitisha magari chn ya reli, l...