Monday, August 25, 2025

MAJALIWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA TEWW





WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Oktoba 25, 2025 ni mgeni rasmi katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Lengo kuu la kongamano hilo ni kuhakikisha kuwa elimu ya watu wazima inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kiteknolojia kwa nchini. Pia ni jukwaa la kubadilishana uzoefu, matokeo ya tafiti na mbinu bora zinazoweza kuendeleza ubunifu katika utoaji wa elimu ya watu wazima.

Kongamano hilo linalofanyika kuanzia leo tarehe Agosti 25, 2025 hadi Agosti 27, 2025 lina kaulimbiu isemayo Elimu Bila Ukomo kwa Maendeleo Endelevu."

 

Rais Samia Aongoza Wito wa Amani na Upendo kuelekea Uchaguzi Mkuu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025.






Matukio mbalimbali kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiombewa dua na watoto yatima wa Kituo cha Watoto Yatima Mburahati mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025 kwa ajili ya kushiriki kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA).





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani, mshikamano na upendo miongoni mwa Watanzania wote kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Akihutubia katika Kongamano la Amani lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) tarehe 24 Agosti 2025, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Rais Samia alisisitiza kuwa Tanzania imejengwa kwa msingi wa mshikamano na kwamba kila mmoja ana jukumu la kuilinda amani hiyo.

Mara baada ya kuwasili ukumbini, Rais alipokelewa kwa heshima kubwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali. Pia, alipata baraka za kipekee kutoka kwa watoto yatima wa Kituo cha Mburahati waliomwombea dua, ishara ya mshikamano wa upendo na mshikikano wa kijamii. Tukio hilo lilionekana kugusa mioyo ya waliohudhuria, likiwa kielelezo cha mshikamano wa vizazi na matabaka mbalimbali ya jamii.

Kongamano hilo lilikutanisha viongozi wa dini, wadau wa siasa, asasi za kiraia na wananchi kutoka makundi mbalimbali kwa lengo la kujenga maelewano na mshikikano wa kitaifa kuelekea uchaguzi. Kwa pamoja walitoa wito wa kudumisha utamaduni wa majadiliano, kuheshimiana na kushirikiana kwa maslahi ya Taifa.

Rais Samia alisisitiza kuwa amani si suala la serikali pekee, bali ni jukumu la kila Mtanzania. Alihimiza vijana, wanawake, viongozi wa dini na wanasiasa kushiriki kikamilifu katika kudumisha mshikamano, kwani Tanzania imekuwa mfano wa amani barani Afrika na duniani kote.

Kwa ujumla, tukio hilo limekuwa chachu ya kuimarisha mshikikano wa kitaifa, huku ujumbe wa msingi ukiwa ni amani na upendo, kama msingi wa maendeleo endelevu na mustakabali wa taifa.


 

Saturday, August 23, 2025

Rais Samia Aongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM Taifa Jijini Dodoma








Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza kikao muhimu cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (CC) kilichofanyika jijini Dodoma, tarehe 23 Agosti, 2025.

Kikao hiki kimehudhuriwa na wajumbe wote wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, ambapo kimejadili masuala mbalimbali ya kisera, kiuongozi na kimaendeleo yanayolenga kuimarisha zaidi uhai wa chama, utekelezaji wa ilani ya uchaguzi pamoja na mipango ya maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Miongoni mwa mambo yaliyopewa kipaumbele katika kikao hicho ni pamoja na:

  • Uteuzi wa wagombea Ubunge kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao, ambapo vigezo vya uadilifu, ufanisi na uwezo wa kusimamia maslahi ya wananchi vilisisitizwa.
  • Mapitio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020–2025, ikiwemo tathmini ya miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia.
  • Mikakati ya kisiasa na kiuongozi kwa ajili ya kuhakikisha chama kinabaki imara, chenye mshikamani na chenye kuendelea kuwa karibu na wananchi.

Katika kikao hicho, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa viongozi wa chama na Serikali kusimamia vyema utekelezaji wa mipango ya maendeleo, kuhakikisha uwajibikaji, utawala bora na uadilifu, ili kuendeleza imani ya wananchi kwa Chama cha Mapinduzi.

Aidha, ametoa rai kwa wanachama na viongozi wote wa chama hicho kuendelea kushirikiana kwa karibu na wananchi katika kutatua changamoto zao, na kuhakikisha CCM inaendelea kuwa kimbilio na chaguo la Watanzania.

Kikao hiki cha Kamati Kuu cha Agosti 23, 2025 jijini Dodoma, kinatajwa kuwa na umuhimu mkubwa katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu, pamoja na kutoa dira na mwelekeo wa chama kuelekea utekelezaji wa mikakati mipya ya maendeleo ya Taifa.

Friday, August 22, 2025

Kaimu Mkurugenzi Mbarali Apokea Mkataba wa Ujenzi wa Kiwanda cha Kuchakata Mafuta ya Alizeti








Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, Bi. Gloria Komba, amepokea rasmi mkataba wa ujenzi wa jengo la kuchakata mafuta ya alizeti lililopo katika Kijiji cha Nyangulu, kutoka kwa Mratibu wa Mradi wa Urejeshwaji Endelevu wa Mazingira na Hifadhi ya Bayanuai Tanzania (SLR), Dkt. Damas Mapunda.

Mradi wa SLR, unaosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais, unalenga kurejesha mazingira yaliyoharibika, kuboresha mifumo ya ikolojia, na kuendeleza maisha bora ya jamii zinazozunguka maeneo yanayotekelezwa miradi hii. Kiwanda hiki cha kuchakata mafuta ya alizeti kitakuwa ni kipengele muhimu cha kuimarisha kilimo cha alizeti na kuongeza kipato kwa wakulima wadogo wa kijiji cha Nyangulu na maeneo jirani.

Makabidhiano ya mkataba yamefanyika leo, Agosti 22, 2025, wakati wa ziara ya wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Ofisi ya Makamu wa Rais, waliotembelea wilaya ya Mbarali ili kujionea miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya Mradi wa SLR. Ziara hii imekuwa fursa ya kuthibitisha jinsi miradi ya kiasili na ya maendeleo ya kijamii inavyotekelezwa, ikiwapa wadau na viongozi fursa ya kuona matokeo ya uwekezaji na juhudi za kurejesha mazingira na kuimarisha ustawi wa jamii.

Mradi wa SLR unadhihirisha azma ya serikali ya kuendeleza miradi endelevu ya mazingira, huku ukiwa ni mfano wa ushirikiano kati ya serikali, jamii na wadau wa maendeleo katika kuhakikisha maendeleo ya kiikolojia na kijamii yanapatikana kwa usawa.

MGODI WA DHAHABU WA GEITA KUWALIPA FIDIA WANANCHI KUPISHA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI




📍Geita.

Serikali imetangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa ulipaji fidia kwa wananchi wa Mitaa ya Nyakabale na Nyamalembo katika Halmashauri ya Manispaa ya Geita, ili kupisha shughuli za uchimbaji wa dhahabu katika Mgodi wa Geita Gold Mining Limited (GGML). Hatua inayoleta suluhu ya mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 26. 

Akizungumza  Agosti 21, 2025 Mkoani Geita, Waziri wa Madini, Mhe.Anthony Mavunde, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekuwa ikifuatilia kwa karibu changamoto za wananchi wa Geita na kutoa maelekezo mahsusi kuhakikisha zinatatuliwa kwa ufanisi.

 “Nawashukuru sana wananchi kwa uvumilivu wenu kwa zaidi ya miongo miwili. Leo hii tunatangaza suluhu ya mgogoro huu kwa sababu Serikali yenu inawajali na Rais wetu amekuwa mstari wa mbele kutaka wananchi wapate haki zao bila usumbufu,” amesema Waziri Mavunde.

Mhe. Mavunde amebainisha kuwa GGML wameridhia kuanza mchakato wa kuwalipa fidia wananchi wa eneo la Nyakabale na Nyamalembo kwa mujibu wa utaratibu ili kupisha shughuli za mgodi. Amesema kuanzia kesho Agosti 22, 2005,  timu ya wataalamu wa Serikali itaanza kazi ya uthamini wa mali, na ndani ya siku 40 tathmini hiyo itakamilika ili wananchi waweze kulipwa stahiki zao.

Aidha, Waziri ameeleza kuwa, mgogoro huo ulikuwa na hoja 13 za msingi ambazo zilihitaji kushughulikiwa, ambapo ndani ya mwaka mmoja na miezi mitatu Serikali kwa kushirikiana na wadau imefanikiwa kutatua hoja 10 kati ya hizo na hatimaye leo kutatua hoja nyingine mbili.

Aidha, Waziri Mavunde ameeleza kuwa, katika jitihada hizo, GGML imekubali kurekebisha mipaka yake ya leseni ya uchimbaji lna kuliachia eneo linalobaki kwa ajili ya wakazi wa maeneo hayo.

“Ninawapongeza viongozi wote mlioshiriki, hususan Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martin Shigella, na timu maalum iliyoundwa kushughulikia jambo hili kwa ufanisi mkubwa wamefanya kazi ya kupitia maoni ya wananchi na kuleta maoni ya wakazi hawa,  bila juhudi zao leo hii tusingefikia hatua hii” amesisitiza Mavunde. 

Pia, Waziri Mavunde ametumia nafasi hiyo kuwaonya na kuwakumbusha wananchi kuepuka tabia ya ‘tegesha’ kwani inaweza kukwamisha zoezi la tathmini na ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaostahili kupata haki zao kwa wakati na kuleta usumbufu kwa mwekezaji na wananchi. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martin Shigella, amemshukuru Rais Dkt. Samia kwa kufuatilia kwa karibu mgogoro huo wa muda mrefu, na kumpongeza Waziri Mavunde kwa kusimamia utekelezaji kwa umakini.

“Wananchi wa Geita wamevumilia kwa muda mrefu. Tunawashukuru kwa ustahimilivu wao na tunahakikisha maelekezo ya Serikali yanatekelezwa ipasavyo kwa manufaa ya wote,” alisema Shigella.

Wananchi wanaotarajiwa kufanyiwa tathmini na kulipwa fidia ni wa mitaa ya Nyakabale na Nyamalembo ndani ya Manispaa ya Geita.

Hatua hiyo ya Serikali inatazamwa kama historia muhimu ya kumaliza mgogoro wa muda mrefu kwa zaidi ya miaka 26 na uliokuwa unachangia sintofahamu kati ya wananchi na mwekezaji, na sasa inaleta matumaini ya maendeleo na mshikamano endelevu katika Mkoa wa Geita.

Thursday, August 21, 2025

Rais Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha CCM chaguo la wagombea bunge






Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kilichofanyika leo, Agosti 21, 2025, Jijini Dodoma.

Kikao hiki kililenga kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za kisiasa, ikiwa ni pamoja na:

  • Wagombea Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

  • Wabunge wa Viti Maalum,

  • Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, na

  • Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Viti Maalum.

Rais Samia Suluhu Hassan aliwashirikisha wajumbe wa kikao hiki mchakato wa kikatiba na uwajibikaji wa kuchagua wagombea wenye sifa bora, ili kuhakikisha uwakilishi unaoendana na matarajio ya wananchi na maendeleo ya taifa.

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AMPONGEZA NDEJEMBI, AMSIFIA KWA UADILIFU NA UCHAPAKAZI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba , amempongeza Mhe. Deogratius John Ndejembi kwa kuaminiwa ...