Saturday, March 22, 2025

KILELE CHA WIKI YA MAJI NA UZINDUZI WA SERA YA MAJI YA MWAKA 2022 TOLEO 2025















Viongozi mbalimbali wamewasili katika kilele cha Wiki ya Maji, sambamba na Uzinduzi wa Sera ya Maji ya Mwaka 2022 (Toleo la 2025), hafla inayofanyika leo Machi 22, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika tukio hili ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ataongoza uzinduzi wa sera hiyo muhimu kwa maendeleo ya sekta ya maji nchini.

Tukio hili linahudhuriwa na viongozi wa Serikali, wadau wa sekta ya maji, wanazuoni, na washirika wa maendeleo, wakijadili mustakabali wa usimamizi na matumizi endelevu ya rasilimali za maji kwa ustawi wa Taifa.

📸 Picha na: Emmanuel Mbatilo

#WikiYaMaji2025 #SeraYaMaji #MajiNiUhai #SamiaSuluhuHassan


No comments:

BILIONI 51 KUTUMIKA UJENZI WA BARABARA, MASOKO NA STENDI JIJINI ARUSHA

Mradi wa Uendelezaji wa Miji na Majiji Tanzania (TACTIC) unatekeleza miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 51 katika Jiji la Arusha ikiwa...