Monday, March 03, 2025

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA YATOA ELIMU KWA WANANCHI ZAIDI YA ELFU 14 BAGAMOYO

 





VICTOR MASANGU, BAGAMOYO

Zaidi ya wananchi elfu 14 kutoka kata nane zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani kutoka katika makundi mbali mbali waliokuwa wanakabiliwa na changamoto mbali mbali katika masuala  ya ndoa, mirathi, migogoro ya ardhi, pamoja na ukatili wa kijinsia  wamepata mkombozi baada ya kupatiwa   msaada  wa kisheria  bure wa Mama Samia  kwa lengo la kuweza kutambua haki zao za msingi.
 
Hayo yamebainishwa na Wakiri George Molel  ambaye ni  mratibu  wa huduma ya  kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama  Samia katika Halmashauri ya Bagamoyo ambapo amesema kwamba  lengo kubwa la msaada huo wa kisheria ni kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ambayo itawasaidia wananchi kujua haki zao za msingi katika masuala mbali mbali.
Wakiri George amebainisha kwamba katika kampeni hiyo ya msaada wa kisheria Katika Halmashauri ya Bagamoyo imeweza kufanikiwa  kupitika katika kata nane, zikiwemo Fukayose,Makurunge, Yombo, Kiromo,Kerege, Nianjema, Kisutu, pamoja na Kata ya Dunda ambapo wameweza kutoa elimu kwa wanafunzi, walimu, wananchi wa kawaida, makanishani pamoja  na makundi mbali mbali.
“Kampeni hii ya msaada wa kisheria ya Mama Samia imeanzishwa  maalumu kwa lengo  la kuweza kuwasaidia wananchi hasa wa hali ya chini kupata msaada wa kisheria kutoka kwa wataalamu mbali  mbali kutoka Halmashauri pamoja na baadhi ya mawakiri kutoka Wizaraya Katiba na sheria na kwamba  msaada huo unatolewa bila malipo yoyote lengo ikiwa ni kuwasaidia wananchi,”amesema Wakiri George.
Kwa upande wake Afisa maendeleo ya Jamii Kata ya Kerege Lilian Mkosyange amesema kuwepo kwa chanagmoto mbali mbali  kwa wananchi ikiwemo suala la  wakinababa  kuwa na tabia ya kutelekeza familia zao na kupelekea mama na watoto kubaki peke yao bila msaada wowote.
Naye mmoja wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo Samweli Ringo  amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuanzisha kampeni hiyo na kubainisha  kwamba elimu ambayo wameipata  itakwenda kuwa mkombozi mkubwa kwani wameweza kujifunza  mambo mbali mbali  juu ya  msaada wa  kisheria.
Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia inaendelea  kufanyika katika  Mkoa wa Pwani ambapo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo tayari imeshapita katika kata zipatazo nane na kutoa msaada wa kisheria katika masuala ya Ndoa, mirathi,migogoro ya ardhi, wosia,matunzo ya watoto,kesi za madai,unyanyasaji wa kijinsia, pamoja na haki za binadamu na mambo mengine ya kimsingi yanayohitaji msaada huo.

No comments:

WAZIRI NA NAIBU WAZIRI WA ARDHI WASHIRIKI KIKAO CHA KWANZA CHA MKUTANO WA 19 WA BUNGE LA 12 KWA AJILI YA KUJADILI BAJETI YA SERIKALI 2025/2026

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi (MB), leo tarehe 8 Aprili 2025, ameshiriki kikao cha kwanza cha Mku...