Thursday, November 09, 2017

NEWZ ALERT:WAZIRI WA KILIMO DKT TIZEBA AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI MKUU WA BODI YA SUKARI TANZANIA


Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Ndg Henry J. Semwanza.


Na Mathias Canal, Dodoma

Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba amemuagiza Katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe kumsimamisha kazi mara moja Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Ndg Henry J. Semwanza kuanzia leo Novemba 9, 2017.

Kwa agizo hilo lililotolewa na Waziri wa Kilimo Dkt Tizeba, Mkurugenzi huyo atatakiwa kurejea kwa mwajiri wake ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo kwa ajili ya kupangiwa kazi nyingine.

Simwanza anasimamishwa kazi kutokana na mwenendo wake wa utendaji akiwa Msimamizi Mkuu wa Bodi ya Sukari kutoridhisha.Simwanza amehudumu katika nafasi hiyo akiwa Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari tangu mwaka 2011.

No comments:

Slovakia Yafungua Ubalozi Tanzania

Balozi Mteule wa kwanza wa Slovakia nchini Tanzania, Mhe. Ivan Lančarič amewasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Naibu Waziri wa Mambo...