Frederick Katulanda wa Mwananchi anaripoti kuwa madiwani watatu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamejeruhiwa baada ya msafara wa Waziri Mkuu kupata ajali na magari matatu kugongana.
Ajali hiyo imetokea majira majira ya saa 4:45 asubuhi katika barabara ya Nkirizya wakati Waziri Mkuu akitokea uwanja wa ndege kuelekea mjini Nansio.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Zelothe Steven alithibitisha kuwepo kwa ajali hiyo na kueleza kuwa chanzo ni vumbi.
Magari yaliyogongana ni Toyota Landcruiser STJ 3292 mali ya Tamesa lililokuwa likiendeshwa na Barnabas Dioniz, T 686 ANU mali ya Meneja wa TRA wilayani hapa lililokuwa likiendeshwa na Chacha Kamene pamoja na Toyota Hiace T428 AAD ambalo lilikuwa na madiwani.
Madiwani walioumia na kujeruhiwa ni Juma Mbasa wa kata ya Ilugwa, Bernard Polisi kata wa Kagunguli na Cypriani Nabigambo wa kata ya Bwiro. Madiwani hao wametibiwa na kuendelea na ziara. Chanzo ni vumbi na magari kuwa karibu karibu.
Naye Thobias Mwanakatwe wa PST, Chunya, anaripoti kuwa Msafara wa NaibuWaziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bi. Mwantum Mahiza jana ulipata ajali baada ya gari waliokuwa wakisafiria kugongwa na lori.
Msafari huo ulikuwa na maofisa wa Idara ya Ukaguzi Nyanda za Juu,waandishi wa habari na askari.Ajali hiyo ilitokea juzi 11:45 jioni katika kijiji cha Luwanjilowilayani Chunya Mkoani Mbeya wakati msafara huo ukitokea katika ziaramjini Chunya kurudi Mbeya mjini.
Lori hilo lenye namba za usajili T 683 AFK liligonga gari lenye nambaSTK 3170 ambalo lilikuwa likiongoza msafara wa Naibu Waziri huyo likiendeshwa na dereva Abel Mwakatete likiwa limewabeba maofisa hao.
Maofisa wa Idara ya Ukaguzi waliokuwa katika gari hilo lililogogwa niNaibu Mkaguzi wa Kanda, Mama Arevo, Mkuu wa shule ya Sekondari Tukuyu,Bw. Wakili Mwangoka, mwandishi wa habari wa RTD na mwandishi wa habariwa Kampuni ya The Guardian, Bw. Thobias Mwanakatwe pamoja na askari,Sajenti Seif ambao hata hivyo hawakujeruhiwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma
Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya mazungumzo na Fitch Ratings Ltd amb...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...
No comments:
Post a Comment