Monday, November 28, 2011

Tamasha la Str8t Music lafana Dar

Fabolous akifanya makamuzi
Sehemu ya nyomi iliyohudhuria
Sehemu ya nyomi iliyohudhuria
Naseeb Abdul ‘Diamond’ akiwajibika. Picha zote ni za Venance Nestory wa Mwananchi.

TAMASHA la Str8Muzik Festival Inter-College Special 2011 la vyuo kwa mwaka 2011 lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam, Jumamosi na kuhudhuriwa na maelfu ya watu, limefana vilivyo.

Kwa muda wa saa tano, tamasha hilo lilipambwa na nyota wa Hip Hop wa Marekani, Fabulous aliyewarusha vijana wa kike na kiume wanaopenda burudani kadri muda ulivyoyoyoma.

Kundi la kwanza kutumbuza kwenye tamasha hilo lilikuwa ni Alleluyah lililokuja na free-style, ambalo lilivumbuliwa katika tamasha kama hilo lililofanyika mwaka
jana.

Fabulous alipanda stejini saa nne na kufanya vitu vyake na kuimba ngoma 20 zinazopendwa na mashabiki.

Baadaye ndipo ukaja wakati wa wanamuziki nguli wa Bongo Fleva waliopanda jukwaani kuanza na kundi la Manzese Crew, Inspekta Haroun, Amani Temba 'Mheshimiwa Temba' na Chege nao walikamua kwa ngoma zao.

Elius Barnaba alikuja akiwa na kundi lake la THT
pia Mfalme wa Rhyme, Afande Sele alipata wasaa wake wa kupiga shoo akifuatiwa na Pina wa Kikosi cha Mizinga alikamua ngoma mbalimbali pamoja na ngoma yake ya Umoja ni Nguvu na kuungwa mkono na wapenzi wa muziki waliokuwa wanamshangilia na kudhihirisha kuwa rapu si tu kwa Fabolous, bali hata kwa Wabongo.

Nao wana-Hip Hop kutoka Arusha Nako 2 Nako waliruka stejini na baadaye kupigwa tafu na wakali Jo Makini na Niki wa Pili.

Usiku huo ulipambwa pia na MwanaFa, Shetta,Diamond Platinum, Big Boy Baghad, Juma Nature, Mchizi Mox na Jay Mo walikamua
na kuwapagawisha wapenzi na sauti zao.

Tamasha la StrMuzik lilianzishwa mwaka 2005 na baadaye lilijulikana kama Inter-College Bash, na kufanyika Dar es Salaam na mwaka 2008 lilifika
hadi Mwanza, Morogoro na Dodoma.

1 comment:

Vimax Pills said...

i like this blog and information, thanks for sharing