Tuesday, November 22, 2011

CASTLE LAGER KUDHAMINI KUONYESHWA KWA MICHUANO YA LIGI KUU YA BARCLAYS AFRIKA

Premier League Fans Playing Games During Launch of Castle Lager's Perfect Moment Premier League Promotion.

Marian Ntuah Picking her T Shirt she won during Castle Lager's Premier League Perfect Moment Promotion.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Castle Lager inadhamini kuonyeshwa kwa michuano ya ligi kuu ya uingereza ya Barclays kwenye vituo vya luninga katika nchi 48 barani Afrika. Shuhudia bia yako ya Castle ikionyesha klabu kubwa za ulaya zikichuana live, wachezaji bora na kukuacha ukishangilia timu uipendayo.

Hii ni mara ya pili mfululizo kwa Castle Lager kudhamini kuonyeshwa live kwa michuano hii ya ligi kuu ya barani ulaya katika vituo vya luninga barani Afrika.

Ni sehemu ya kusaidia uendeshwaji matukio ya michezo katika bara zima na kufanya kila muda kuwa muafaka - hata kama utatazama michuano hii ukiwa nyumbani na rafiki zako kadhaa.

Mashabiki wapenzi wa soka watapata nafasi ya kuangalia timu nne zenye kiwango cha juu. Timu hizo ni kama Manchester United, Liverpool, Chelsea na Arsenal zitachuana katika ligi kuu ya Uingereza ya Barclays kila jumamosi katika michuano hiyo itakayoendelea.

Bia yako ya Castle imekuwa ikitoa mchango mkubwa katika soka kwa kipindi cha zaidi ya miaka 30 ikiwa inadhamini Baraza la chama cha soka cha Afrika ya kusini (COSAFA) Michuano mkubwa, Kombe la Kagame Castle Tanzania na ligi kuu maarufu ya Soka nchini Afrika ya kusini.

Meneja wa kinywaji cha Castle Lager, Bi Kabula anasema “Castle Lager kwa makusudi imechagua vituo vingi vya luninga vitakavyosaidia michuano kuonwa na watazamaji wengi zaidi.

Amesema pia “kujihusisha kwa kinywaji cha Castle Lager katika kudhamini mpira wa miguu inatokana na wao kutambua mapenzi ya wateja wao”. “Tukiwa tunashirikiana na michuano hii ya ligi kuu ya Uingereza tunakiweka kinywaji chetu katika sehemu nzuri barani Afrika,” Alisema.

Bi. Kabula anasema pia kwamba Castle Lager ina mipango ya kuanziasha vitu vya kusisimua zaidi mwaka huu. “Kwahiyo iwe utatazamia michuano hii katika baa uipendayo au nyumbani ukiwa unachoma nyama na marafiki zako, hakikisha kila tukio linakuwa la uhakika ukiwa na Castle Lager yako mkononi. Bia yenye ladha kamili itakayokuwanya ukate kiu yako."

Kama sehemu ya mipango hii, Castle Lager pia imezindua promosheni ambayo itawawezesha wateja wa Castle Lager kujishindia zawadi mbalimbali wakienda kwenye baa au watakaponunua chupa ya Castle Lager.

Baa maalum zitakuwa na mabango ya Castle Lager yakiwa na namba maalum za kuscan. Wateja wataweza kuscan namba hizo kwa kutumia simu zao za mkononi, ambazo tovuti ya www.theperfectmoment.mobi itafunguka na kuwawezesha kucheza mpira wa miguu ndani ya tovuti hiyo na kujishindia zawadi mbalimbali.

Wateja ambao pia watanunua Castle Lager bia katika baa watapatiwa kadi ambayo ina namba maalum ambayo wataweza kutuma ujumbe mfupi kwenda namba fulani na kujishindia zawadi mbalimbali.

1 comment:

Foto Cewek Bugil said...

i like it this blog and article