Monday, November 28, 2011

Sugu afanya vitu vyake viwanja vya Ustawi wa Jamii


Mr II akiwa jukwaani na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika. Wabunge takribani wanane walisindikiza uzinduzi wake huo ulioenda sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachoeleza historia yake katika maendelea ya muziki wa Rap Bongo.
Msanii Mr II Sugu akifanya vitu vyake usiku wa kuamkia jana kwenye viwanja vya Ustawi wa Jamii
Mheshimiwa Mbunge Joseph akiwa anachana mistari jukwaani usiku wa kuamkia jana, nyomi ilikuwa ya kutisha
**********************************

Boniface Meena

MKALI wa muziki wa Hiphop nchini, Joseph Mbilinyi maarufu kama 'Sugu' usiku wa kuamkia jana akisindikizwa jukwaani na wabunge kadhaa, aliteka nyoyo za maelfu wa mashabiki wa sanaa ya muziki waliofurika kushuhudia uzinduzi wa albamu yake mpya iliyopewa jina la 'Anti Virus' kwenye viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii, Jijini Dar es Salaam.
Sugu ambaye pia ni mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), alifunika tamasha hilo kwa kuimba nyimbo zake za zilizowateka kimawazo mashabiki wake wengi vijana.
Kivutio kikubwa kwenye onyesho hilo, alikuwa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye alipanda jukwaani na kuwasalimia mashabiki: "Oyoooo Oyoooo...nimefurahi kupanda jukwaani kucheza pamoja nanyi."
Katika onyesho hilo lililopambwa na burudani kutoka vikundi mbalimbali vya muziki wa kizazi cha wakati huu (Bongo Fleva), Sugu pia aliimba na kucheza sambamba na wabunge wenzake kama John Mnyika, Joyce Mukya na Regia Mtema na Highness Samson.
"Oyoooo...Oyoooo. Nawashukuruni sana kwa kutuunga mkono, leo nauweka pembeni uheshimiwa na kushusha mawe. Pigeni kelele mpaka walioko Leaders Club wasikie," alisema Sugu.
Baada ya salamu hizo, alianza kwa kuimba wimbo wa 'Sugu Moto Chini' ambao uliwaamsha mashabiki kwa furaha, kisha akachombeza mashairi kadhaa ya wimbo 'Yamenikuta' na kupiga wimbo mwingine 'Kiburi' aliomshirikisha Stara Thomas.
Hakuishia hapo, akaimba wimbo mwingine 'Mambo ya Fedha', 'hayakuwa mapenzi' na mwisho akateremsha wimbo wenye jina la 'Sugu' ambao uliwapa utumwa wa kushangilia bila kuchoka mashabiki wake.
Kabla ya kushuka jukwaani Sugu alisema yuko mbioni kufanya wimbo na kumshirikisha mwenyekiti wake Mbowe.
Katika uzinduzi huo Sugu alisindikizwa na wasanii kama Danny Msimamo, Mabaga Fresh, Adili na Soggy Doggy Hunter, Mgosi Mkoloni, Mapacha, Suma G, Zay B na wengine wengi.

3 comments:

Anonymous said...

Very balanced journalism. Wewe ndugu yangu huwaogopi akina Ruge? Wenzako wakina Michuzi Jr hawaweki pichaza Sugu maana wana-kiss Ruge na Clouds' asses. Labda ndio maana blogs zao zinamatangazo mengi. Heri utumwa wa mwili kuliko wa akili. Big up ndugu yangu usichoke utafika.

Pelangsing cepat said...

thanks to nice blog and good sharing

Vimax Asli said...

i like this blog and information