Sunday, November 27, 2011

JK akutana na Chadema

Rais Jakaya Kikwete, akimkaribisha mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Ikulu jijini Dar es salaam muda mfupi uliopita leo. (picha: K-VIS blog)


Ujumbe wa CHADEMA ukijongea lango la Ikulu

Rais Kikwete anakabidhiwa kabrasha la mapendekezo

Picha ya pamoja ya viongozi wa pande zote mbili
Mbowe na JK

RAIS Jakaya Kikwete jana alikutana na ujumbe wa Chadema kukabidhiwa kabrasha la mapendekezo yao na kujadili mchakato wa utungwaji wa Katiba mpya.

Rais alikutana na viongozi hao majira ya saa tisa na nusu alasiri mpaka saa 12 jioni na kukabidhiwa kabrasha la maoni ya viongozi hao kabla ya viongozi hao walioongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, kupiga picha za pamoja na Rais wakiwa ndani na baadaye nje ya jengo la Ikulu na hatimaye kuendelea na majadiliano.

Mbowe alilieleza Mwananchi kwamba kikao chao hicho cha majadiliano kilidumu kwa saa tatu na kiliahirishwa saa 12 jioni na kitaendelea kesho asubuhi saa nne.

"Ndugu waandishi wa habari tumekutana na Rais na baadhi ya mawaziri na Wasaidizi wake! Kikao kilianza saa 9:30 mchana na kiliahirishwa saa 12 jioni. Kikao kitaendelea kesho asubuhi saa nne. Taarifa kamili ni baada ya kikao,"alieleza Mbowe katika ujumbe wake kwa vyombo vya habari.

Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lisu, ambaye alikuwa Katibu wa Kamati hiyo wakati wa mkutano huo na John Mrema. Katibu Mkuu Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwapo.

No comments: