Monday, December 29, 2008

Kubenea akiwa na Paschal


MKURUGENZI Mtendaji wa gazeti la MwanaHALISI (ambalo liko kifungoni), Saed Kubenea mwenye miwani, akimjulia hali mwanahabari Pascal Mayala jana katika hospitari ya Apollo Indraprastha, mjini Delih nchini India.

Mayala amelazwa hopitari hapo akipata matibu yaliotokana na ajali ya pikipiki miezi mitatu iliyopita ambapo alijeruhiwa vibaya mguu wa kushoto, mkono wa kushoto na bega la kushoto.

Kwa upande wake, Kubenea yupo nchini India kwa takribani mwezi mmoja sasa, akipata matibabu ya macho yaliotokana na kuvamiwa na kumwagiwa tindikali, ofisini kwake Januari 05 mwaka huu.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PPR, Pascal Mayala akiwa amelazwa katika Hospitali ya Apollo Indraprastha, mjini Delhi nchini India anakotibiwa baada ya kujeruhiwa vibaya katika ajali ya pikipiki iliyotokea hivi karibuni nchini.

Picha na (mpiga maalum)

3 comments:

Anonymous said...

Pole sana kaka Pascal Mayalla kwa ajali mbaya ya pikipiki uliyoipata ukiwa Tanzania. Tunamshukuru mwenyezi Mungu alikunusuru. Mungu akutie nguvu na upone haraka na kurudi nyumbani kuendelea na shughuli zako. Get Well Soon brother Pascal.

Mdada.

Evarist Chahali said...

Aisee imepita muda mrefu kiasi kwamba baadhi yetu tulishasahau kuhusu ajali aliyopata Paschal.Asante kwa kutu-update kuhusu hali yake na usichoke kutujulisha maendeleo ya afya yake.Sala zetu ni miongoni mwa tiba kwa tunaoamini,hivyo ikibandikwa picha hapa anapata sala mbalimbali za kumwombea apone haraka.

A Khudori Soleh said...

salam from khudori