Wednesday, August 30, 2017

Serikali Yaanza kukabidhi Leseni kwa Kwa Machapisho

PIX0
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi leseni ya usajili wa Gazeti la Daily News mwakilishi wa gazeti hilo Bi. Pudenciana Temba. Idara ya Habari imetoa imetoa leseni nne kwa ambapo leseni namba moja imetolewa kwa Jarida la Nchi Yetu linalotolewa na Idara hiyo, namba mbili imetolewa kwa HabariLeo, namba tatu Dailynews na nne imetolewa kwa Spotileo.Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Usajili Bw. Patrick Kipangula.
PIX1
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi leseni ya usajili wa Gazeti la HabariLeo mwakilishi wa gazeti hilo mhariri wa gazeti hilo Bw. Amir Mhando leo Jijini Dar es Salaam. Leseni hiyo imetolewa kufuatia kuanza kwa matumizi ya sheria mpya ya Huduma za Habari ya mwaka 2016.
PIX2
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News, HabariLeo na SpotiLeo Dkt. Jim Yonaz akisisitiza jambo mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kutolewa kwa Leseni za magazeti ya Kampuni yake kumalizika leo Jijini Dar es Salaam.
PIX3
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimpongeza Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News, HabariLeo na SpotiLeo, Dkt. Jim Yonaz kwa Kampuni yake kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016  kwa kujisajili upya na kupatiwa leseni.
PIX4
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa magazeti ya HabariLeo, DailyNews, SpotiLeo yanayomilikiwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) pamoja na uongozi wa Idara ya Habari (MAELEZO) mara baada ya kukabidhiwa Lesini za usajili wa magzeti hayo leo Jijini Dar es Salaam.
Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO
…………………….
Na. Neema Mathias na Paschal Dotto- MAELEZO.
Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO) imeanza rasmi utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari kwa kutoa leseni kwa vyombo vya machapisho yakiwemo Magazeti na Majarida.  
Akizungumza katika makabidhiano ya leseni hizo Jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi amesema  utoaji wa leseni ni utekelezaji wa agizo rasmi lililotolewa Agosti 23, 2017 lililowataka wamiliki wote wa machapisho kujisajili upya na kupewa leseni kwa lengo la kuifanya tasnia ya Habari kuwa taaluma rasmi kama zingine.
“Leseni hizo zimeanza kutolewa rasmi Agosti 23 na zoezi hilo litaendelea hadi Oktoba 15, 2017 na baada ya hapo wale amabo watachapisha magazeti  na majarida bila kuzingatia Sheria hiyo watakuwa wametenda kosa la jinai”, alisema Dkt. Abasi.
Katika zoezi hilo Dkt. Abbasi alitoa leseni kwa vyombo vinne ambavyo ni Jarida la Nchi Yetu linalomilikiwa na Idara ya Habari MAELEZO, gazeti la Daily News, Habari Leo pamoja na Spoti Leo ambayo ni magazeti ya Serikali.
Dkt. Abbasi ametoa wito kwa vyombo vingine vya habari ambavyo bado havijaanza taratibu za upataji wa leseni visisubiri hadi dakika za mwisho za mchakato huo ili kuepuka msongamano na usumbufu usio wa lazima.
“Nitumie fursa hii kuwaalika ambao hawajapata leseni wafanye haraka, Tanzania Standard Newspaper (TSN) walitimiza masharti ndani ya siku tatu ndio maana leo wamepata leseni hizo, hakuna urasimu wala nia mbaya ya kufungia baadhi ya machapisho kama wengi wanavyodai bali ni katika kutekeleza matakwa ya Sheria”, alisisitiza Dkt. Abbasi.
Kwa upande wake Mhariri Mtendaji wa TSN Dkt. Jim Yonazi ameviasa Vyombo vingine vya Habari kutekeleza agizo hilo ili kupata uhuru mpana katika uwajibikaji pamoja na kuwa mfano wa kutii Sheria bila shuruti ili taaluma ya habari iendelee kuheshimika kwa jamii.
“Ukifanya kazi kihalali unakuwa na uhuru wa kufanya kazi vizuri, ubunifu unaongezeka na unafanya biashara bila wasiwasi”, alisisitiza Dkt.Yonazi.

Dawasa kujenga miundombinu ya majitaka jijini Dar es Salaam

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam, Mhandisi Romanus Mwang’ingo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari juu ya mikakati Dawasa ya maji safi na majitaka jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maelezo, Rodney Thadeus kulia ni Meneja Mawasiliano Dawasa, Neli Msuya.
Meneja wa Mawasiliano wa Dawasa, Neli Msuya akizungumza juu miradi inajengwa na Dawasa katika maeneo mbalimbali Dar es Salaam na Sehemu ya mkoa wa Pwani  jijini Dar es Salaam.

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.

UZALISHAJI wa Maji Safi kunahitaji kuwepo na miundombinu ya maji taka ambayo yanazalishwa na maji safi katika kutunza mazingira pamoja na afya kwa wananchi wanatumia maji safi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam, Mhandisi Romanus Mwang’ingo amesema kuwa wameanza kufanya utekelezaji wa miradi ya ukusaji na uondoshaji wa majitaka kwa kuanzisha miradi mitatu ya kisasa ya kusafisha majitaka hayo.

Amesema Miradi hiyo itakwenda sambasamba na uzalishaji wa mabomba ya kukusanya majitaka hayo kwa kujenga miundombinu katika maeneo ya Jangwani, Mbezi Beach pamoja na Kurasini.

Mwandisi Mwang’ingo amesema ujenzi wa miundombinu hiyo itaongeza kiwango cha kusafisha majitaka kwa asilimia 30 ifikapo 2020 kutoka kiwango cha asilimia 10 iliyopo sasa itakayogharimu Dola za Kimarekani Milioni 600 katika mwaka wa fedha 2017/2018.

Amesema mfumo wa majitaka wa Jangwani utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kusafisha majitaka hayo mita za ujazo 200,000 kwa siku.

Mabomba yenye urefu wa kilomita 376 yatajengwa katika mradi utakaonzia kunazia Ubungo hadi Jangwani,Kinondoni, Mwananyamala, Msasani Katikati ya Jiji na Ilala.

Mhandisi Mwang’ingo amesema kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi itahusisha sehemu sehemu itakayoweza kusafisha mita za ujazo 25,000 kwa siku na mabomba yenye urefu wa kilomita 17.43 yatakayojengwa eneo la magomeni.

Aidha katika awamu ya kwanza,bomba linalomwaga majitaka baharini litaacha kutumika na badala yake majitaka hayo yatakwenda kusafishiwa katika mtambo huo ambapo mtambo huu unajengwa kati ya ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Serikali ya Korea kupitia mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Exim ya Korea unaotarajiwa kugharimu Dola za Kimarekani milioni 90 ambazo tayari zimepatikana.

Wakazi wa Shinyanga na Geita kunufaika na uwekezaji mradi wa umeme

Kampuni ya Acacia, kwa ushirikiano na TANESCO, imejenga kituo cha kupozea umeme kilichopo katika mgodi wake wa dhahabu wa Bulyanhulu ambacho kimeweza kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme katika maeneo ya mgodi huo.

Acacia imewekeza shilingi bilioni 5.5 katika mradi huo ambao utanufaisha maeneo yanayozunguka migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu na maeneo mengine ikiwa ni pamoja na Kahama, Shinyanga, Msalala, na sehemu nyingine za Geita.

Ujenzi wa Kituo hicho ulianza Desemba 2016 na unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Haya ni maendeleo makubwa kwa viwanda na biashara zinazozunguka eneo hilo ambazo zitafaidika na uwepo wa umeme wa uhakika jambo litakalosaidia kuboresha ufanisi na kuongeza uzalishaji.

Mkuu wa kitengo cha miradi ya maendeleo wa mgodi wa Bulyanhulu, Jiten Divecha ameeleza kuwa tatizo la mabadiliko ya nguvu ya umeme limekuwepo kwa muda mrefu na limekua likisababisha uharibifu mkubwa wa mashine.“Ujenzi wa kituo hiki utasaidia kupunguza athari zinazotokana na kuongezeka au kupungua kwa nguvu ya umeme katika migodi yetu hivyo kuboresha shughuli za uzalishaji. Wakazi na viwanda vinavyotumia umeme katika wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga na wilaya zingine za mkoa wa Geita zitafaidika na uwekezaji huu pia,” alisema Jiten.

Aliongeza: "Acacia inajitahidi kuleta manufaa ya kiuchumi ya pamoja kwa jamii zinazotuzunguka na wadau wake kupitia miradi endelevu."
Wakati wa ujenzi wa kituo hicho, ajira mbalimbali zilitolewa kwa jamii zinazozunguka mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu.
Akizungumzia fursa hiyo, David Nyanda alisema: “tunathamini sana ujenzi wa mradi huu kwa sababu tumepata fursa za ajira. Japokuwa fursa hizi ni za muda, tunaweza kupata mapato ili kuendesha familia zetu hasa katika kipindi hiki cha ukame.”

NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA AFANYA ZIARA MKOANI GEITA, ASISITIZA UKUSANYAJI WA MAPATO YA ARDHI NA MAJENGO

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akiangalia ramani ya Kijiji cha Bukandwe ambacho kipo kwenye Wilaya ya Mbongwe Mkoani Geita. Mkuu wa Wilaya ya Mbongwe Mathar Mkupasi akiagana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula wakati alipotembelea kijiji cha Bukandwe. Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ,Josephat Maganga akisoma taarifa fupi ya Wilaya ya Bukombe kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akikagua na kupatiwa maelezo na afisa ardhi mteule Joseph Kimondo . Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula ,akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Bukombe.PICHA ZOTE NA JOEL MADUKA .
 
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula akiwasili kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Geita na akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo Nyuma yake ni mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga 
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akisaini kwenye kitabu cha wageni ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Mbongwe. Mkuu wa Wilaya ya Mbongwe Mathar Mkupasi akisoma taarifa ya ardhi na maendeleo ya ukusanyaji wa mapato ambayo yanatokana na ardhi pamoja majengo yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya Hiyo. Watumishi wa halmashauri ya Mboongwe pamoja na kamati ya Ulinzi na usalama wakifuatilia kikao cha Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe Elias Kayandabila akionesha mchoro na ramani ya nyumba ambazo zinatarajia kujengwa na shirika la Nyumba la Taifa. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe Elias Kayandabila akikabidhi ramani kwa meneja wa shirika la Nyumba Mwanza, Simiyu na Geita Mhandisi Benedict Kilimba . Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akikagua mafaili kwenye ofisi za Ardhi za Wilaya hiyo.

TPA YATOA MSAADA WA MASHUKA 900 KWA HOSPITALI ZA WILAYA YA TEMEKE

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Felix Lyaviva (wanne kushoto) akishukuru kupokea msaada wa Mashuka 900 yenye thamani ya Tshs Milioni 10 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko (watano kushoto)
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Felix Lyaviva (wapili kushoto) akishukuru kupokea msaada wa Mashuka 900 yenye thamani ya Tshs Milioni 10 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng Deusdedit Kakoko (watatu kushoto).

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imetoa msaada wa mashuka 900 yenye thamani ya Sh. Milioni Kumi kwa Hospitali za Temeke, Mbagala Zakheim na Round zilizopo katika Wilaya ya Temeke.

Msaada huo umekabidhiwa leo na Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko kwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Felix Lyaviva ikiwa ni sehemu kutambua na kuthamini dhamira na kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Joseph Magufuli, ya kufikisha huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi wote na hasa wa hali ya chini.

“Menejimenti ya TPA, chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Bodi ya Wakurugenzi ya TPA, inaunga mkono kwa dhati kabisa juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano za kuhakikisha jamii inapata huduma muhimu, TPA inayo Sera ya Misaada kwa Jamii ambayo imejikita katika kusaidia jamii kwenye nyanja za Afya, Elimu na Maendeleo ya Kijamii,” amesema Mhandisi Kakoko.

Mhandisi Kakoko ameongeza kuwa pamoja na kwamba TPA kazi yake kubwa ni kuhudumia shehena mbalimbali zinazopita kwenye bandari zote nchini, lakini pia ina wajibu wa kurudisha kile inachokipata kutokana na huduma zake kwa kuisaidia jamii inayoizunguka na ndio maana imeamua kutoa msaada huo kwa Wilaya hii ya Temeke ilipo Bandari ya Dar es Salaam ambayo kiutendaji ndiyo bandari kubwa kuliko bandari zote hapa nchini.

Hivi karibuni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alizindua rasmi kuanza kwa kazi ya maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam na mara itakapokamilika mwaka 2022 itaiwezesha bandari hiyo kuhudumia meli zenye uwezo wa kubeba kontena 8,000 kutoka kontena 2,500 za sasa na kuiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya ushindani na kuliongezea Taifa mapato.

WANAFUNZI MSALATO GIRLS WAJIPANGA KUINGIA 10 BORA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua maeneo ya vyoo na mifumo ya maji iliyokarabatiwa katika shule ya Sekondari ya wasichana Msalato.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akipata maelezo ya ukarabati wa mabwene kutoka kwa mmoja wa wakandarasi wanaofanya ukarabati huo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa mabweni nane yaliyofanyiwa ukarabati katika shule ya Sekondari ya wasichana.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa shule hiyo pamoja na maafisa wengine wakifanya ukaguzi wa majengo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Msalato Dodoma.
Miongoni mwa mabweni yaliyokarabatiwa na serikali.

Wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya wasichana ya Msalato Manispaa ya Dodoma wamemuahidi Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Mhe. Selemani Jafo kwamba watapambana ili katika matokeo ya kidato cha sita mwakani shule yao iwe miongoni mwa shule kumi bora nchini. 

Ahadi hiyo ilitolewa na wanafunzi hao katika ziara ya Naibu Waziri Jafo alipotembelea shule hiyo kukagua ujenzi wa miundombinu inayojengwa na serikali ili kuirudisha shule hiyo katika hadhi yake.

Shule hiyo ni miongoni mwa shule kongwe 88 zilizo katika mpango wa ukarabatiwa na serikali ambapo ndani ya miaka 4 shule hizo zitakuwa ni shule zenye ubora wa hali ya juu kwa kuboreshewa mazingira yake yakiwemo mabweni, madarasa, vyoo, mabwalo, mifumo ya maji na umeme, pamoja na nyumba za walimu. 

Katika shule hiyo, serikali hadi sasa imeshakamilisha ukarabati wa mabweni nane, mfumo wa umeme na maji.Aidha Serikali imejipanga kuendelea na ukarabati wa madarasa na ujenzi wa madarasa mengine manne mapya, ukarabati wa bwalo la chakula, majengo ya utawala, na nyumba za walimu. 

Kufuatia uboreshaji huo, Wanafunzi wameishukuru serikali na wamemuahidi Naibu Waziri huyo kwamba watahakikisha wanajitahidi ili mwakani shule yao iwe miongoni mwa shule kumi bora katika matokeo ya kidato cha sita.

Akizungumza na wanafunzi hao, Naibu Waziri Jafo amewahakikishi watanzania kwamba mpango wa serikali ni kuboresha shule za umma ili ziweze kutoa elimu bora hapa nchini.Mwaka jana, Naibu Waziri Jafo alitembelea shule hiyo na kuwataka wanafunzi wa kidato cha sita kuhakikisha wanafanya vizuri katika mitihani yao ili shule hiyo itoke kutoka shule ya 21 katika matokeo ya kidato cha sita mwaka jana ili waingie 10 bora. Jambo ambalo katika matokeo ya mwaka huu shule hiyo imeshika nafasi ya namba 14 kitaifa.

Thursday, August 24, 2017

KAMATI YA MAWASILIANO NA UJENZI YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR YAVUTIWA NA UTENDAJI WA NHC

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ambaye ni mwakilishi wa Jimbo la kwa Mtipura, Mhe:Hamza Hassan Juma. Katika Maelezo yake Mheshimiwa Hamza Juma alipongeza utendaji wa kasi wa NHC na kusema ndicho kitu kikubwa kilichowavutia kama Wazanzibari kufika NHC kujifunza na kuchukua fursa hiyo kulipongeza Shirika kwa mchango wake mkubwa wa kuliasisi Shirika la ZHC.




 Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ambaye ni mwakilishi wa Jimbo la kwa Mtipura, Mhe:Hamza Hassan Juma, akizungumza wakati ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar hiyo ulipofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi. 
 Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ambaye ni mwakilishi wa Jimbo la kwa Mtipura, Mhe:Hamza Hassan Juma, akizungumza wakati ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar hiyo ulipofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi. 
Baadhi ya Watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifuatilia kwa karibu maelezo yaliyokuwa yakitolewa katika mkutano huo jana mchana.
Wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifuatilia maelezo katika mkutano huo.
Wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifuatilia maelezo katika mkutano huo.
Baadhi ya Watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa na wengine kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na vyombo vya habari wakifuatilia kwa karibu maelezo yaliyokuwa yakitolewa katika mkutano huo jana mchana.
Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter akitoa maelezo ya miradi kwa ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi.
Wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifuatilia maelezo katika mkutano huo.
Baadhi ya Watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa na wengine kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na vyombo vya habari wakifuatilia kwa karibu maelezo yaliyokuwa yakitolewa katika mkutano huo jana mchana.
Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter akitoa maelezo ya miradi kwa ujumbe wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ambaye ni mwakilishi wa Jimbo la kwa Mtipura, Mhe:Hamza Hassan Juma, akizungumza na vyombo vya habari nje ya mutano huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na vyombo vya habari wakati Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na vyombo vya habari wakati Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliofika katika Shirika la Nyumba la Taifa kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ujenzi, teknolojia mpya na mikakati ianayowezesha kufanyika kazi kwa kasi zaidi.

RUZUKU YA SH.MILIONI 250 YATOLEWA KWA WABUNIFU WA MATUMIZI BORA YA NISHATI

📌 Kamishna wa Umeme asema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana wabunifu katika teknolojia ya matumizi bora ya nishati 📌 Wabunifu wa kike...