Wananchi wa eneo la soko kuu la Manispaa ya Mpanda mjini, Mkoani Katavi wamelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuendesha zoezi la usafi lililofanyika sokoni hapo, ambapo wamesema hatua hiyo imechangia kuboresha mazingira ya biashara na afya ya jamii kwa ujumla.
Zoezi hilo limefanyika Julai 29, 2026 likiongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna msaidizi Mwandamizi (SACP) Kaster Ngonyani ambapo, amesema kuwa zoezi hilo ni endelevu lenye lengo la kuhamasisha wananchi kutunza mazingira huku akiwataka wafanyabiashara na wananchi kuendelea kushirikiana katika kudumisha usafi wa soko na maeneo mengine yanayowazunguka.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa wa Kashaulili Ndugu Johari Korongo amelipongeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa kuonyesha ushirikiano mzuri na wananchi kwa kujitolea na ametoa wito kwa taasisi nyingine kuiga mfano huo kwa kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo na huduma kwa jamii.

.jpeg)


No comments:
Post a Comment