Saturday, February 01, 2025

Rais Samia Akabidhi Mobile Clinic kwa Sikonge na Uyui






Dodoma, 1 Februari 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Matiku Chacha, mfano wa ufunguo wa magari maalum ya huduma ya afya inayotembea (Mobile Clinic) kwa ajili ya Wilaya za Sikonge na Uyui.

Magari hayo yametolewa na Jakaya Kikwete Foundation kwa ufadhili wa Kampuni ya SC Johnson Family ya Marekani, ikiwa ni juhudi za kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa maeneo husika. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

No comments:

KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC), Mhe. Mahmoud Ali Youssouf, amemteua Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Ki...