Saturday, February 01, 2025

CCM ARUSHA WAUNGA MKONO AZIMIO, RAIS SAMIA NA RAIS MWINYI WAGOMBEA PEKEE 2025

 




Na Vero Ignatus,Arusha

MAELFU ya Wananchi wa Mkoa wa Arusha leo Jumamosi Februari 1, 2025 wamejitokeza kwa wingi kwenye tukio la kuunga Mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi la Januari 19, 2025 lililomuidhinisha Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania na Dkt. Hussein Mwinyi wa Zanzibar, kuwa wagombea Urais kupitia CCM katika Uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu.

Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Arusha leo Jumamosi wamefanya Mkutano Mkubwa wa hadhara kwenye viwanja vya Kilombero Jijini Arusha ili kuunga Mkono azimio hilo, wakati huu ambapo Chama hicho tawala kikiendelea na shamrashamra za kuelekea miaka 48 ya kuzaliwa kwake.

No comments:

RAIS NDAITWAH AONDOKA BAADA YA KUKAMILISHA ZIARA YA KITAIFA YA SIKU TATU NCHINI

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Dkt, Netumbo...