Saturday, February 01, 2025

CCM ARUSHA WAUNGA MKONO AZIMIO, RAIS SAMIA NA RAIS MWINYI WAGOMBEA PEKEE 2025

 




Na Vero Ignatus,Arusha

MAELFU ya Wananchi wa Mkoa wa Arusha leo Jumamosi Februari 1, 2025 wamejitokeza kwa wingi kwenye tukio la kuunga Mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi la Januari 19, 2025 lililomuidhinisha Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania na Dkt. Hussein Mwinyi wa Zanzibar, kuwa wagombea Urais kupitia CCM katika Uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu.

Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Arusha leo Jumamosi wamefanya Mkutano Mkubwa wa hadhara kwenye viwanja vya Kilombero Jijini Arusha ili kuunga Mkono azimio hilo, wakati huu ambapo Chama hicho tawala kikiendelea na shamrashamra za kuelekea miaka 48 ya kuzaliwa kwake.

No comments:

Rais Dkt. Samia Awasili Addis Ababa Kushiriki Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi wa AU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bole, Jij...