Monday, October 14, 2024

DKT.TULIA AFUNGA MKUTANO MKUU WA 149 WA UMOJA WA WABUNGE DUNIANI MJINI GENEVA USWISI

 Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 14 Oktoba, 2024 amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa 149 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (CICG) mjini Geneva, Uswisi.

Mkutano huu unalenga kujadili mada kuu inayohusu “Matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa ajili ya mustakabali wa Amani na Uendelevu.” Mkutano huu umehudhuriwa na takribani washiriki 1,500 wakiwemo Maspika, Naibu Maspika, Wakuu wa Misafara pamoja na Wabunge. Mkutano unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 17 Oktoba, 2024 kwa kutoa maazimio muhimu yatakayolenga kutatua changamoto za kimataifa zinazoikabili dunia kwa sasa.


 

No comments:

WANANCHI 216 WAKABIDHIWA HATI MILIKI WILAYANI MASWA

Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Simiyu, leo imeendesha zoezi la kugawa jumla ya hati miliki 216 kwa wananchi wa Wilaya ya Maswa....