Wednesday, November 28, 2018

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LACHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI KISARAWE

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo akielezea sifa za eneo la Vigungu kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani wakati msafara huo wa Mkurugenzi Mkuu ulipokuwa katika eneo la Vigungu kunakotarajiwa kupimwa kwaajili ya uendelezaji wa makazi na shughuli mchanganyiko. Eneo hilo liko katika Barabara kuu iendayo Kibaha na eneo limetenganishwa na viwanda kwa barabara hiyo iendayo Kibaha. Matangi mawili ya kuhifadhia maji, yenye uwezo wa lita milioni tano, yatajengwa katika maeneo ya karibu na hapo, kwa ajili ya viwanda na makazi mapya; na Minarani kwa ajili ya mji wa Kisarawe kwa gharama ya Sh bilioni 10.



Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani akitia saini kwenye kitabu cha wageni cha Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe alipotembelea ofisi hizo kabla ya kutembelea baadhi ya fursa za uwekezaji  wilayani Kisarawe ambapo Shirika la Nyumba la Taifa linaweza kushirikiana na Wilaya hiyo katika uwekezaji maeneo yaliyotembelewa ni pamoja na eneo la  Community Hall,  Stendi ya zamani na eneo kunakotarajiwa kuanza kupimwa viwanja vya makazi na shughuli mchanganyiko la Vigungu lililopo nje kidogo ya mji wa Kisarawe. 


Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akizungumza na ujumbe wa Shirika la Nyumba la Taifa, ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk. Maulidi Banyani. 


Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtela Mwampamba akiukaribisha ujumbe kutoka NHC na kisha kuwatambulisha maafisa watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. 


Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Dk. Maulidi Banyani akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo kuelekea eneo la  Community Hall lililopo jirani kabisa na zilipo Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.


Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Dk. Maulidi Banyani akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo walipotembelea eneo la Stendi ya zamani Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani leo.


Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Dk. Maulidi Banyani akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo walipotembelea eneo la Stendi ya zamani Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani leo.


Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtela Mwampamba akielekeza jambo msafara huo ulipokuwa katika eneo la Vigungu kunakotarajiwa kupimwa kwaajili ya uendelezaji wa makazi na shughuli mchanganyiko eneo hilo liko katika Barabara kuu iendayo Kibaha na eneo limetenganishwa na viwanda kwa barabara hiyo iendayo Kibaha. Matangi mawili ya kuhifadhia maji, yenye uwezo wa lita milioni tano, yatajengwa katika maeneo ya hayo, kwa ajili ya viwandana makazi mapya; na Minarani kwa ajili ya mji wa Kisarawe kwa gharama ya Sh bilioni 10.



Eneo la  Vigungu kunakotarajiwa kupimwa kwaajili ya uendelezaji wa makazi na shughuli mchanganyiko eneo hilo liko katika Barabara kuu iendayo Kibaha na eneo limetenganishwa na viwanda kwa barabara hiyo iendayo Kibaha. Matangi mawili ya kuhifadhia maji, yenye uwezo wa lita milioni tano, yatajengwa katika maeneo yaVigungu, kwa ajili ya viwandana makazi mapya; na Minaranikwa ajili ya mji wa Kisarawe kwagharama ya Sh bilioni 10.


Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani na ujumbe wake akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo kwenye eneo la Vigungu wakati msafara huo wa Mkurugenzi Mkuu ulipokuwa katika eneo la Vigungu kunakotarajiwa kupimwa kwaajili ya uendelezaji wa makazi na shughuli mchanganyiko.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani na ujumbe wake akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo kwenye eneo la Vigungu wakati msafara huo wa Mkurugenzi Mkuu ulipokuwa katika eneo la Vigungu kunakotarajiwa kupimwa kwaajili ya uendelezaji wa makazi na shughuli mchanganyiko.


Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akizungumza na ujumbe wa Shirika la Nyumba la Taifa, ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk. Maulidi Banyani. 


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani na ujumbe wake akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo mbele ya ofisi  ya Mkuu wa Wilaya.



Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo mbele ya ofisi  ya Mkuu wa Wilaya.





Kaimu Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Shirika la Nyumba la Taifa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.


Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.

No comments: