

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIABUNGE LA TANZANIA | ||
Simu Na. 022 2112065 Fax Na. (255) 022 2112538 E-mail: tanzparl@parliament.go.tz (Barua zote za kiofisi ziandikwe kwa (KATIBU WA BUNGE) Unapojibu tafadhali taja: | Ofisi ya Bunge S.L.P. 9133 DAR ES SALAAM |
Kumb. EB.155/172/01/300 31 Mei, 2011
YAH: WANAHABARI KWA AJILI YA BUNGE LA BAJETI
____________________
Tunayo furaha kukujulisha kuwa, Mkutano wa Nne wa Bunge la kumi la Jamhuri ya Muungano wa
Ofisi ya Bunge kila mara imekuwa ikitamani kupata toka kwako Wanahabari wenye uzoefu na uelewa wa kutosha juu ya masuala ya Bunge zikiwemo kanuni na taratibu zinazotawala chombo uendeshaji wa chombo hiki.
Aidha, ili kuwa na uratibu mzuri wa shughuli za utoaji Habari za Bunge, mwaka 2008 Wanahabari waliamua kuunda umoja wao kwa ajili ya kuwaunganisha katika shughuli hizi. Umoja huo uitwao Bunge Press Association of Tanzania (BUPAT) pamoja na mambo mengine unalenga kuwajengea uwezo Wanahabari na uwelewa mpana wa masuala ya Bunge.
Ni nia ya Ofisi ya Bunge kuuendeleza umoja huo ili hatimaye kujenga kada ya Wanahabari waliobobea katika utoaji wa Habari za Bunge. Katika kutekeleza azima hii, ofisi inaandaa mpango wa mafunzo utakaojumuisha semina, warsha na ziara za mafunzo katika Mabunge mbali mbali kwa Wanahabari husika.
Ni kwa misingi hiyo basi tumeona ni vyema tukapata ushirikiano wako katika hili na hivyo kukuomba kuwa kuanzia sasa unapoteua Wanahabari kwa ajili ya kwenda Bungeni wakidhi vigezo vifuatavyo:
Tunatanguliza shukurani zetu za dhati kwa ushirikiano wako katika jambo hili.
Pamoja na salaam toka ofisi za Bunge.
J.S. Mwakasyuka
Kny: KATIBU WA BUNGE
SHIRIKA LA NYUMBA LINAPENDA KUWAJULISHA WAPANGAJI WOTE KWAMBA KUANZIA TAREHE 01 JULAI, 2011 OFISI YA SHIRIKA LA NYUMBA ILIYOKO UPANGA ITAHAMISHIWA PLOT NO. 568/48 MTAA WA SAMORA, JENGO LA MATSALAMAT, GHOROFA YA KWANZA.
AIDHA HUDUMA ZOTE ZINAZOHUSU WAPANGAJI ZITATOLEWA KWENYE OFISI MPYA KUANZIA JULAI 01, 2011. WATEJA WATAENDELEA KULIPIA KODI YA PANGO KWENYE OFISI ZETU ZILIZOPO MTAA WA NKRUMAH.
TAWI LA UPANGA NI KUBWA KULIKO MATAWI YOTE YA SHIRIKA NA LINAHUDUMIA WAPANGAJI WENGI HIVYO NI VYEMA KUWA NA OFISI AMBAYO WATEJA WETU WATAPA HUDUMA ZENYE UBORA ZAIDI.
TUMEONA NI VYEMA KUWAARIFU WAPANGAJI WETU MAPEMA ILI KUWAONDOLEA USUMBUFU USIOKUWA WA LAZIMA.
KWA KUONA UMUHIMU WA SUALA LA MAKAZI SHIRIKA LIMEONA NI VYEMA KUTUMIA KIKAMILIFU THAMANI YA ARDHI ILIYOPO KATIKA ENEO HILI ILI KUWEZA KUWAPATIA WANANCHI MAKAZI ZAIDI.
JENGO LITAKALOJENGWA HAPA LITAKUWA NA SEHEMU ZA KUISHI TAKRIBAN 200 HIVYO WATU 1000 WATANUFAIKA KUISHI KATIKA ENEO HILI LITAKALOKUWA NA MIUNDOMBINU MUHIMU NA HUDUMA ZINGINE ZA KIJAMII KAMA VILE MADUKA, SEHEMU ZA KUCHEZA WATOTO, SEHEMU ZA KUEGESHA MAGARI NA KADHALIKA. HII NI KATIKA KUTEKELEZA AZMA YA KILIBADILISHA KABISA ENEO LA UPANGA.
KWA SASA ENEO LA UPANGA LINA WAPANGAJI 4,772 NA MAKUSANYO YA MWEZI NI ZAIDI YA SHILINGI BILIONI MOJA AMBAPO NI KARIBU ASILIMIA 40 YA MAKUSANYO YA KODI KATIKA MIKOA YOTE.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA
Na Sixmund Begashe - Serengeti Ziara ya kikazi ya watafiti wa mimea vamizi kutoka Jamhuri ya Cuba walioungana na wataalam wa ikolojia kutok...