Tuesday, July 17, 2007

Waziri Meghji, hebu tukuulize swali

NIMEPITIA magazeti ya wiki hii nikakuta habari zinazoonekana kama nzito hivi, zinanivutia kichwa chake cha habari, najaribu kuzisoma kwa undani na hata umakini kutokana na kunigusa kwa kiasi kikubwa.

Habari hizo zinazungumzia hatua inazozichukua serikali kunusuru hali mbaya inayoelezwa kusababishwa na wauzaji mafuta.

Nikadhani ni habari moto na nzito hasa. Namaliza kuzisoma naishia kutikisa kichwa. Nasikitika hasa mimi mvuja jasho , nasikitikia wavuja jasho wenzangu wengi tu waliotapakaa hapa nchini wanaoishi kwa taabu na uchungu wakitamani kupotea katika uso wa dunia.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...